Habari Kali
Loading...

Picha: Raisi Magufuli Amtembelea Maalim Seif katika Hoteli ya Serena kwa ajili ya kumjuilia hali yake.

Rais Magufuli akisalimiana naKatibu mkuu waCUF Maalim Seif Sharif Hamad   ndani  ya  Serena  Hoteli  alipoenda  kumjulia  hali  leo march 9
Rais Magufuli akisalimiana naKatibu mkuu waCUF Maalim Seif Sharif Hamad   ndani  ya  Serena  Hoteli  alipoenda  kumjulia  hali  leo march 9

Unaweza kuyatazama hapa matokeo yote ya kidato cha nne 2015/16

Baraza la mitiani Tanzania NECTA limetangaza Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2015 , ambapo  ufaulu  unaelezwa kushuka  kwa 1.85%  toka  69.75%  mwaka 2014  hadi 67.91%  mwaka  2015.
Matokeo yote unaweza kuyatazama >>HAPA

Sentensi sita za NECTA kuhusu matokeo ya mitihani ya kidato cha nne 2015

February 18 baraza la mitihani Tanzania NECTA wametangaza matokeo ya kidato cha nne kwa mwaka 2015 yafuatayo ni maneno matatu waliyosemwa na katibu mtendaji wa baraza la mitihani Tanzania NECTA Dk Charles Msonde.
“Katika mkutano maalum wa baraza wa 110 uliofanyika February 17 2016, baraza la mitihani Tanzania lilipitia taarifa ya matokeo ya kidato cha nne na maarifa uliofanyika tarehe 2 hadi 27 November 2015 na kuidhinisha kutangaza rasmi kwa matokeo hayo katika mitihani ya kidato cha nne 2015”
“Jumla ya watahiniwa 448382 waliandikishwa kufanya mtihani huo, wasichana ni 229144 na wavulana 219238 kati ya hao watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 394o65, wakati watahiniwa wa kujitegemea walikuwa 54317”
“Watahiniwa wa shule asilimia 96.71 walifanya mitihani na watahiniwa 14749 ambao sawa na asilimia 3.29 hawakufanya mtihani, watahiniwa wa kujitegemea 49333 sawa na asilimia 90.82 lakini watahiniwa 4984 sawa na asilimia 9.18 hawakufanya mtihani”
“Watahiniwa wa mtihani wa maarifa 19547 waliosajiliwa, lakini watahiniwa kati ya wale waliosajili 16162 sawa na asilimia 82.68 walifanya mtihani, lakini watahiniwa 3385 kati ya hao hawakufanya mtihani”
“Kwa jumla ya watahiniwa 272947 sawa na asilimia 67.53 ya watahiniwa waliofanya mtihani wa kidato cha nne wamefaulu mtihani, wasichana waliofaulu ni 131913 sawa na asilimia 64.84, wakati wavulana waliofaulu ni 141034 sawa na asilimia 71.09”
“lakini mwaka jana watahiniwa waliofaulu walikuwa  196805 sawa na asilimia 68. 33 hivyo ufaulu ukilinganisha na matokeo ya mwaka jana, ufaulu umeshuka kwa asilimia 0.8 ukilinganisha na matokeo ya mwaka 2014”

Unaweza kuyatazama matokeo yote ya kidato cha pili 2015/16

Tayari Serikali kupitia Baraza la mitiani NECTA imetangaza Matokeo ya kidato cha pili mwaka 2015  324,068 sawa na 89% kati ya wanafunzi 363,666 waliofanya mtihani wamefaulu kuendelea na kidato cha tatu kwa mwaka 2016.
Matokeo yote unaweza kuyatazama hapa>>http://www.necta.go.tz/matokeo/ftna2015/html/index.htm

Jipya la Dr. Shein kuhusu uchaguzi mkuu Zanzibar na mengine…(+Audio)

Leo Jan 12 2016  Zanzibar ilikuwa ikiadhimisha miaka 52 ya mapinduzi,  ambapo Rais Dr. Ali Mohamed Shein alipata time ya kuwahutubia wananchi wake na haya ndio aliyoyalenga zaidi.

VIDEO: Rais John Pombe Magufuli akiwaapisha Makatibu Wakuu na Manaibu Katibu Wakuu, Ikulu Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Pombe Magufuli akiwaapisha Makatibu Wakuu pamoja na Manaibu Katibu Wakuu Ikulu Jijini Dar es Salaam, 01 Januari, 2016.

Wananchi Kupanga Nauli za Mabasi Yaendayo Kasi


MAMLAKA ya Udhibiti,Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), inatarajia kukusanya maoni ya wananchi juu ya viwango vya nauli za mabasi yatakayotoa huduma ya usafiri wa haraka Jijini Dar es Salaam.

Taarifa hiyo imetolewa na Ofisi ya Mkurugenzi wa SUMATRA kwa vyombo vya habari kwenda kwa wananchi  ambapo ofisi hiyo itawaalika wadau wote wa usafiri hususani wananchi kuchangia maoni kwenye mkutano utakao fanyika januari 5 kwenye ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam kuanzia saa 3 na nusu asubuhi.

Mamlaka  pia inapokea maoni ya wananchi kupitia anuani ya ofisi ya Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka hiyo ambayo ni S.L.P 3093 au kwa barua pepe ambayo info@sumatra.go.tz ambapo kabla ya kufikia uamuzi wadau wanatakiwa kutoa maoni ya kuridhia viwango vya nauli  kwa mujibu wa sheria ya Sumatra.

Maoni ya maandisi yatapokelewa kwenye ofisi ya Mkuregenzi Mkuu iliyopo Jengo la Mawasiliano House Makutano ya barabara ya Ali Hassani Mwinyi na Nkumo kuanzia Saa 4 asubuhi hadi saa 9 alasiri mwisho wa kupokelewa maoni hayo ni Januari 13 mwaka huu.

Mamlaka hiyo imepokea maombi ya nauli kutoka kampuni ya UDA-RT inayolenga kutoa huduma ya mpito ya usafirishaji jijini Dar es Salaam katika kutekeleza awamu ya kwanza ya mradi wa Dart.

Maombi yaliyowasilishwa na kampuni hiyo ni Safari kwenye njia za pembeni (feeder route) shilingi 700 ,safari kwenye njia kuu (trunk route) shilingi 1200 na njia zote mbili ni 1400 ambapo wanafunzi watalipa nusu nauli anayotoa mtu mzima.
Mpekuzi blog

Mwigulu Nchemba Atumbua Mtu JIPU Machinjio ya Pugu.......Ni Baada ya Kufanya Ziara Jana Usiku na Kurudi Tena Leo Asubuhi

Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Mh. Mwigulu Lameck Nchemba, amemfukuza kazi mkuu wa mnada wa mifugo wa Pugu, na watumishi walioshiriki kuiba ushuru wa serikali, alipoenda machinjioni hapo kukagua.

Waziri Nchemba amesema alienda machinjioni hapo kutatua kero zinazowakabili wananchi na wadau wa machinjio hayo, huku akishirikisha wizara mbili ya Afya na TAMISEMI.

“Nimerejea asubuhi ya leo kwenye machinjio ya Vingunguti kwa ajili ya kutatua kero zinazowakabili watumiaji wa machinjio hayo, kutokana na uwepo wa ubadhilifu wa kodi ya serikali kwenye mnada wa pugu na malalamiko kadhaa yanayogusa wananchi wanaotumia machinjio haya, nimeshirikisha wizara mbili (TAMISEMI na AFYA) kutoa majawabu ya muda mfupi na ya kudumu”, alisema Waziri Nchemba

Baada ya kufika machinjioni hapo Waziri Mwigulu Nchemba alitoa maagizo kwamba Mkuu wa mnada wa machinjioni hapo watafute kazi nyingine, na kuwataka kufika ofisi ya Katibu Mkuu wa wizara.

“Nimeagiza kuwa Mkuu wa mnada wa Pugu na watumishi waliokuwa zamu tar. 24.12.2015 na tar.01.01.2016, kuanzia sasa watafute kazi nyigine, wakati huohuo wahakikishe wanafika ofisi ya Katibu mkuu wizarani kwangu mapema Jumatatu tar.04/01/2016”, alisema Waziri Nchemba.

Pamoja na hayo Waziri Nchemba amesitisha uchukuaji wa ushuru katika eneo la mnada wa Pugu, na kutaka makusanyo ya fedha zote yafanyike machinjio ya Vingunguti kwa kutumia mashine za EFD.

“Kuanzia sasa nimesitisha uchukuaji wa ushuru eneo la mnada wa Pugu, badala yake makusanyo yote ya fedha za serikali yatafanyika machinjio ya Vingunguti kwa kutumia mashine za elektroniki za EFD, kwa maana hiyo mnada wa Pugu utakuwa unatumika kutoa vibali tu vya mifugo ilikudhibiti ubora wa mifugo inayopaswa kuchinjw”, alisema Waziri Nchemba.

Pia waziri Nchemba ametaka eneo la kuhifadhia nyama lililokuwa limejengwa kwa fedha za wananchi kushirikiana na serikali lifunguliwe kwa ajili ya wananchi kulitumia kuhifadhia nyama.

Hatua za kuboresha miundombinu ya machinjio hayo zimeelekezwa kwa Halmashauri ya Ilala zifanyiwe kazi haraka na kwa ubora, na kutakiwa kurudishwa kwa umeme uliokuwa umekatwa eneo hilo, kwa ajili ya kuwarahisishia wananchi shughuli zao.
Mh:Mwigulu Nchemba akiwa ameambatana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI Mh:Simbachawene wakiwasili kwenye eneo la machinjio ya Vingunguti kwaajili ya kutoa majawabu kutokana na kero mbalimbali zinazowakabili wadau wa machinjio hayo.[​IMG][​IMG]Mwigulu Nchemba akiwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI Mh:Simbachawene wakikagua eneo la machinjio ya Vingunguti kabla ya kuzungumza na wadau wa eneo hilo pamoja na uongozi wake.

[​IMG]Mh:Mwigulu Nchemba akiwa ameongozana na Mh:Simbachawene wakielekea kuzungumza na wananchi wanaotumia Machinjio ya vingunguti.[​IMG]Mawaziri kutoka kulia ni Naibu waziri wa Afya Mh:Kigwangallah,Wa pili kutoka kulia ni Mbunge wa Jimbo la Segerea Mh:Bonah,Watatu kutoka kulia ni Mh:Simbachawene na wa mwisho kushoto ni Mh:Mwigulu Nchemba wakijadiliana jambo.[​IMG]Mkutano ukiendelea wa kutoa majawabu kuhusu changamoto za Machinjio ya Vingunguti.[​IMG]Mh:Simbachawene akiwaagiza watumishi wote wa Machinjio ya Vingunguti kuripoti ofisini kwake Jumanne wakiwa na mkurugenzi wa Manispaa ya Ilala.[​IMG]Mh:Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi(Wadau) wa machinjio ya Vingunguti kuhusu hatua za kinidhamu alizozichukua kwa Mkuu wa mnada wa pugu inakotoka mifugo kabla ya kufika Machinjio ya Vingunguti kwa upotevu wa mamilioni ya shilingi ya kodi za serikali.[​IMG]Mawaziri wakiagana na wananchi mara baada ya mkutano wa kutatua kero zao za Machinjio kumalizika.[​IMG]Furaha ya Wananchi mara baada ya kutatuliwa kero zao kwa hatua za awali,wananchi wanasukuma gari la Mh:Mwigulu Nchemba kama ishara ya kukubali hatua alizochukua.

Ufisadi Mwingine Wa Bilioni 48 Waibuliwa Bandarini .......7 Watiwa Mbaroni, 8 Wanasakwa na Jeshi la Polisi

Serikali imepoteza jumla ya Sh48.47bilioni baada ya makontena 11,884 na magari 2,019 kupitishwa badarini Dar es Salaam bila kulipiwa kodi.
 
Hata hivyo, jumla ya watu saba wanashikiliwa na wengine nane wanatafutwa na Jeshi la Polisi kwa kuhusishwa na ukwepaji kodi huo uliolikosesha taifa mapato.
 
Akizungumza na wanahabari leo jijini Dar es Salaam, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema ufisadi huo umebainika baada ya serikali kuzifanyia ukaguzi bandari zote za nchi kavu (ICDs) jijini Dar es Salaam.
 
Akifafanua, Waziri Mbarawa amesema makontena hayo 11,884 yalikuwa na thamani ya Sh 47.4 bilioni wakati magari gari 2019 zenye thamani ya sh 1.07bilioni yalitolewa bandarini pasipo kulipiwa tozo.

Makontena hayo yalitolewa katika bandari kavu ni MOFED 61, DICD 491, JEFAG 1, 450, AZAM 295, PMM  779, AMI 4384, TRH 4,424 ambazo kodi yake ni zaidi ya sh.bilioni 47.

Magari 2019 yalitolewa bila kulipa kodi katika kampuni za  TALL 309, CHICASA 65, FARION 18, SILVER 97, MASS 171, HESU 1359 na kunyima nchi kodi yenye thamani zaidi ya Tsh.bilioni moja (1).
 
Waliotiwa mbaroni na jeshi la polisi baada ya kukamatwa  leo ni John Elisante, Leticia Masaro, Christina Temu, Merina Chawala, Adnan Ally ,Masoud Seleman na Benadeta Sangawe.

Wanaotafutwa kwa tuhuma za kusababisha upotevu wa kodi za serikali katika bandari ya Dar es Salaam ni Happygod Naftal, Nathan Edward, Aron Lusingu, Amani Kazumari, John Mushi, Valentine Sangawe, Benasweet Kamaina, Zainab Bwijo.
Mpekuzi blog

Maombi ya Kupandisha Ada Yatinga Wizarani

Shule nyingi za msingi na sekondari zisizo za Serikali, zimetuma maombi kwa Kamishna Mkuu wa Elimu nchini kuomba kibali cha kupandisha ada katika mwaka ujao wa masomo.

Hatua hiyo ni kuitikia amri ya Serikali ya kuzipiga marufuku shule binafsi, kupandisha ada kiholela na badala yake shule zote zinatakiwa kuwasilisha maombi ya kupandisha ada hiyo mpya kwa kamishna huyo ili yajadiliwe.

“Kwa kweli baada ya tangazo lile shule nyingi zimeleta maombi yao hapa na kilichobaki ni kwa kamishna wa elimu kuhakikisha anapitia maombi hayo kwa kuzingatia vigezo mbalimbali vilivyowekwa na Serikali,” alisema Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Sifuni Mchome .

Alisema lengo la maombi hayo ni kuondoa tabia ya wamiliki wa shule zisizo za Serikali, kupandisha ovyo ada kwa kadiri wanavyotaka, jambo lililosababisha shule nyingine kugeuza elimu kuwa biashara badala ya kutoa huduma.

Lengo la wizara hiyo ya kutaka maombi hayo na kiwango cha ada wanazotoza kwa sasa ni kubaini shule, ambazo zinafanya biashara na zile ambazo zinatoa huduma ya elimu kwa kuisaidia Serikali. Shule ambazo zitabainika kufanya biashara, zitatakiwa kulipa kodi kutokana na biashara hiyo wanayoifanya.

Profesa Mchome aliwataka wazazi kuisaidia Serikali kwa shule ambazo hazitafuata utaratibu huo, watoe taarifa kwa halmashauri za wilaya, wizarani ili kuhakikisha zile ambazo zimekaidi agizo hilo, zinachukuliwa hatua.

“Hizi shule ni nyingi ziko zaidi ya 1,000, naomba wazazi watusaidie kwa shule ambazo zitakaidi agizo la Serikali watuletee taarifa ili tuweze kuchukua hatua kwa shule husika,” alisema Profesa Mchome ambaye alisisitiza kuwa wazazi wafanye vikao na shule husika kuhusu upandishwaji ambao unatangazwa na shule husika.

Alisema maombi ya kupandisha ada ambayo yanawasilishwa kwa Kamishna wa Elimu, yanaweza kukubaliwa au kukataliwa kulingana na hoja mbalimbali ikiwemo ukubali wa wazazi baada ya kufanya kikao cha uongozi wa shule, huduma inayotolewa na shule husika.

Nia ya Serikali ni kuhakikisha kuwa upatikanaji wa elimu unaendana na uwezo wa wananchi na viwango vilivyokubaliwa.
Mpekuzi blog

MBOWE AHUKUMIWA, UTATA WA SIFA YA KUGOMBEA WAIBUKA

Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe akizungumza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Hai, Kilimanjaro jana mara baada ya kulipa faini ya shilingi milioni moja na kuachiwa huru ,hukumu iliyotokana na kutiwa hatiani kwa kosa la kumshambulia mwangalizi wa uchaguzi mwaka 2010.
MWENYEKITI wa Chadema, Freeman Mbowe amehukumiwa kulipa faini ya Sh1 milioni au kwenda jela mwaka mmoja baada ya kupatikana na hatia ya kumshambulia mwangalizi wa Uchaguzi Mkuu mwaka 2010.
Freeman Mbowe.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi wa Wilaya ya Hai, Denis Mpelembwa. Mbowe, ambaye ni Mbunge wa Hai alilipa faini hiyo iliyochangwa chapchap na wabunge saba wa Chadema na wafuasi wa chama hicho waliokuwa mahakamani hapo.

Wabunge waliochanga fedha hizo ni, Mustafa Akuney wa Mbulu Lucy Owenya, Grace Kiwelu, Cecilia Pareso, Joyce Mukya, Rose Kalili na Paulin Gekul wote wa Viti Maalumu.

Utata wa kupoteza sifa ya kugombea
Hukumu hiyo iliibua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii juu ya uwezekano wa kumzuia Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni kuwania tena ubunge au urais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.

Hata hivyo, Mwanasheria, Alex Mgongolwa akinukuu Katiba ya Tanzania Ibara ya 67 (1)(c); 67(2) (c na d) alisema hukumu hiyo haiwezi kumzuia kugombea ubunge kwa sababu hakwenda jela na kosa lake halihusu kukosa utovu wa uaminifu, kukwepa kodi wala kuvunja Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma.

Suala hilo linafanana na lililotokea katika mchakato wa uteuzi wa wagombea urais mwaka 2005 wakati aliyekuwa mgombea urais wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila na mgombea mwenza wake, Saidi Soud Said walipowekewa pingamizi kutokana na kutumikia kifungo jela, Mtikila akitumikia mwaka mmoja kwa kosa la uchochezi, Said akitumikia chuo cha mafunzo kwa kosa la biashara ya vitambaa. Hata hivyo, pingamizi hilo lilitupwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame (marehemu) baada ya kusikiliza utetezi wa Mtikila na Said, kuwa makosa waliyofungwa kwayo hayakuwa ya kukwepa kodi, kukosa uaminifu wala kukiuka maadili ya viongozi wa umma.

Mashtaka
Mbowe alikuwa anakabiliwa na mashtaka ya kumfanyia shambulio la kawaida, mwangalizi wa ndani wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 31, 2010, Nassir Yamin katika kituo cha kupigia kura kilichokuwa katika Zahanati ya Lambo.

Yamin alikuwa ni mwangalizi wa kutoka Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (Bakwata).

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mpelembwa ambaye amehamishiwa Bukoba, alisema kitendo kilichofanywa na Mbowe hakikubaliki na kinapaswa kukemewa.

“Kitendo alichokifanya mshtakiwa akiwa Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema na Mbunge wa Jimbo la Hai ambaye alipaswa kuwa kioo cha jamii hakikubaliki na lazima kikemewe,” alisema.
“Kwa hiyo hukumu ya Mahakama ni kwamba atalipa faini ya Sh1,000,000 au akishindwa kulipa atakwenda magereza kwa mwaka mmoja,” alisema hakimu huyo.

Ushahidi
Akichambua ushahidi uliomtia Mbowe hatiani, Hakimu huyo alisema Mahakama imeegemea ushahidi wa shahidi wa kwanza, Yamin na shahidi wa pili John Mushi aliyekuwa msimamizi wa kituo.

Alisema ushahidi huo ulieleza kuwa siku hiyo Mbowe aliingia katika Kituo cha Zahanati ya Lambo katika Jimbo la Hai na kuuliza uhalali wa mlalamikaji kuwapo kituoni hapo.

Mashahidi hao waliiambia Mahakama kuwa walimuona Mbowe akimkunja na kumtoa nje kwa nguvu mwangalizi huyo wa ndani na baadaye mbunge huyo kuondoka katika kituo hicho.

Alisema ushahidi wa mashahidi hao uliungwa mkono na shahidi wa nne wa mashtaka, ambaye ni daktari wa Hospitali ya Wilaya ya Hai, aliyemtibu mlalamikaji na kujaza fomu PF3.

Alisema ushahidi wa daktari huyo unaonyesha kuwa mlalamikaji alikuwa na michubuko katika shavu lake moja na shingoni iliyotokana na kupigwa na kitu butu.

Hata hivyo, aliukataa ushahidi wa shahidi wa saba, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi, Shafii aliyekuwa mpelelezi mkuu kuwa Mbowe alikiri kufanya kosa hilo alipoandika maelezo ya onyo polisi.

Hakimu Mpelembwa alisema japokuwa upande wa mashtaka uliwasilisha maelezo hayo kama kielelezo lakini baada ya kuyapitia, hakuna mahali ambako Mbowe alikiri kufanya kosa hilo.

Utetezi wa Mbowe
Hakimu Mpelembwa alisema wakati akijitetea mahakamani, Mbowe alikanusha kufanya tukio hilo lakini alikiri kufika katika kituo hicho na kumtaka mwangalizi huyo kumwonyesha kitambulisho chake.

“Katika utetezi wake, mshtakiwa alikanusha kumpiga Nasir Yamin wala kumfanyia kitu chochote kibaya, bali alimwamuru atoke nje kwani hakuwamo kwenye orodha ya waangalizi iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.”

Hakimu huyo alisema, Mbowe alieleza kuwa hakuwahi kuitwa polisi, bali alikwenda mwenyewe baada ya kusikia kwenye vyombo vya habari kuwa amefunguliwa kesi ya aina hiyo.

Sababu za kutiwa hatiani
Hakimu Mpelembwa alifafanua dhana ya kosa la shambulio kuwa ni kitendo chochote chenye nia ya kudhuru mtu mwingine au hata kujaribu tu kumdhuru au kumtia hofu.

“Kwa maana nyingine ni kitendo cha kumtia mtu mwingine hofu na ili kosa hilo litimie ni lazima mshtakiwa awe na nia isiyo halali kisheria ya kutaka kutenda kosa nililolianisha,” alisema.

Hata hivyo, hakimu huyo alisema shahidi wa kwanza (Yamin) na wa Pili (msimamizi) waliiambia Mahakama kuwa mshtakiwa alimkunja na kumvuta nje mlalamikaji atoke nje ya kituo.

“Ushahidi wa Yamin na Mushi ni wa kuona kuwa mshtakiwa alimkunja na kumtoa nje mlalamikaji. Swali hapa ni je, kumvuta mtu na kumtoa nje kunapelekea kosa la shambulio?” alihoji.

Hakimu huyo alisema kwa tafsiri ya dhana nzima ya kosa la shambulio ni dhahiri kitendo alichokifanya mshtakiwa kinaangukia katika kosa hilo kwa mujibu wa sheria.

“Ushahidi wa shahidi wa kwanza na wa pili wa upande wa mashtaka unashabihiana na ushahidi wa daktari kwamba kulikuwa na michubuko. Kwa mantiki hiyo Mahakama inakubali ushahidi huo. Kutokana na Mahakama kukubali ushahidi wa mashahidi hao watatu, inakutia hatiani kwa kosa la shambulio kama ulivyoshtakiwa nalo.”

Mwendesha mashtaka, Inspekta Msaidizi wa Polisi, Feo Simon alisema ingawa hawana kumbukumbu ya makosa ya nyuma ya mshtakiwa, aliiomba itoe adhabu kali ili iwe fundisho kwake na kwa jamii.

Wakili wa Mbowe, Issa Rajabu aliyekuwa akisaidiana na Albert Msando, aliomba Mahakama impe adhabu ndogo mteja wake kwani hajawahi kutenda kosa lolote la jinai.

Hata hivyo, Hakimu Mpelembwa alisema kwa kutoa adhabu ya faini ya Sh1 milioni au kifungo cha mwaka mmoja jela amezingatia ombi la wakili wa Mbowe.

Baada ya hukumu
Hukumu hiyo iliyoanza saa sita mchana hadi saa 7.20 mchana, wafuasi wa Chadema waliokuwa wamefurika mahakamani hapo walitandika kanga chini na kuanza kuchangishana faini hiyo kazi ambayo ilisimamiwa na Kiwelu.

Wakati kazi hiyo ikiendelea, Mbowe aliendelea kushikiliwa ndani ya chumba cha Mahakama hadi wabunge hao walipokwenda Benki ya NMB, Tawi la Hai saa 7.40 mchana na kulipa faini hiyo na Mbowe kuachiwa saa nane mchana.

Mbowe azungumzia hukumu
Akizungumza nje ya chumba cha Mahakama hiyo, Mbowe aliwatoa hofu wanachama wa Chadema kwamba wasikatishwe tamaa na hukumu hiyo ambayo alisema alitegemea ingekuwa hivyo.

“Mnanipa pole ya nini? Kuna msiba hapa? Tupeane hongera. Sikutarajia cha tofauti na hiki kilichofanyika. Hakinivunji nguvu, bali kinaniimarisha katika mapambano,” alisema.

“Haki katika nchi hii itapiganiwa kwa watu wengine kuumia na wengine kuokoka. Nimesota mahakamani miaka mitano badala ya kufanya kazi ya wananchi. Hainivunji moyo,” alisema na kuongeza:

“Hainivunji moyo katika azma yangu ya kuikomboa nchi hii na ukombozi uko jirani. Mahakama ya nchi hii vimekuwa ni vyombo vya kutoa dhuluma kwa wananchi japo siyo mahakimu wote. Lakini iko siku Mahakama zitakuwa ni sehemu ya kutolea haki, kutenda haki na haki ionekane imetendeka. Mapambano yanaendelea na nawaomba msiwe wanyonge,” alisisitiza.

“Sitaki kuizungumzia Mahakama katika hatua ya sasa lakini ndani ya Mahakama kuna watu wanaotenda haki na ndani ya Mahakama kuna watu wasiotenda haki,” alisema Mbowe.

Alisema kesi hiyo haikustahili kuiendesha kwa miaka mitano na kwamba kodi za wananchi zinateketea pamoja na muda, akisema haiwezekani nchi ikaendeshwa katika utaratibu huo.

“Kama mimi mbunge, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, mtunga sheria wa nchi hii naweza kusoteshwa mahakamani miaka mitano, mwananchi wa kawaida atafanywaje?” alihoji Mbowe.
(CHANZO: GAZETI LA MWANANCHI, ALHAMISI, JUNI18  2015)

GOOD NEWS: Majambazi Matatu (3) Yauawa na Jeshi la Polisi Mkoani Kigoma


JESHI  la Polisi Mkoani Kigoma limefanikiwa kuuwa majambazi watatu baada ya kurushiana risasi na kukamata silaha mbalimbali za kivita.

Akizungumzia tukio hilo ofisini kwake Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kigoma,Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Frednand Mtui alisema kuwa majira ya saa nane usiku katika eneo la  mto kahabwe mpakani mwa Wilaya ya Kakonko na Kibondo, askari Polisi wakiwa doria walirushiana risasi na majambazi ambao idadi yao haijajuikana na kufanikiwa kuwauwa majambazi watatu.

Alisema wamefanikiwa kukamata silaha moja aina ya AK.47 yenye namba 10363 ikiwa na risasi 11 ndani ya magazine na risasi 22 za SMG ndani ya mfuko wa rambo pamoja na mabomu 2 ya kutupa kwa mkono .

Kamanda Mtui alisema kuwa aina ya mabomu waliyokutwa nayo majambazi hao ni offensive handgrenade namba Y.3PM-2 na jingine ni aina  ya deffensive handgrenade ambalo namba zake hazisomeki.

''Leo ilikuwa ni siku ya mnada hivyo inaonekana majambazi hao walijipanga kwenda kupora mali na pesa katika mnada wa leo,tunawashukuru raia wema kwa kutoa taarifa mapema na kufanikiwa kuwanasa majambazi hao na kuwauwa''alisema Kamanda Mtui

Alisema maiti za majambazi wote watatu ambao majina yao hayajafahamika ila wote wana umri kati ya miaka 25-35 zimehifadhiwa katika Wilaya ya Kibondo na upelelezi wa tukio hilo unaendelea.

Rais Kikwete Azindua Meli Mbili Za KIVITA Kwa Kishindo Jijini Dar


RAIS Jakaya Kikwete, jana amezindua na kuzitunukia Kamisheni meli mbili za kivita za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Kamandi ya Wanamaji ambazo zitatumika kufanya doria na kulinda mipaka ya majini katika Bahari ya Hindi.

Meli hizo zimepewa majina ya P77 Mwitongo na P78 Msoga zenye urefu wa mita 60 na zina uwezo wa kufanya doria katika kina kirefu cha maji.

Rais Kikwete alisema, kupatikana kwa meli hizo kumeifanya Tanzania kuandika ukurasa mpya wa uhusiano kati yake na China ambao uliasisiwa na waasisi wa mataifa hayo hayati Mwalimu Nyerere na Mao Tse Tung.

Alisema meli hizo zimekuja nchini kwa msaada wa Serikali ya Watu wa China zikiwa na uwezo wa kubeba silaha nzito kila moja ikiwa na mizinga miwili mikubwa na midogo sita.

"Jeshi letu la Wanamaji wakati linaanzishwa 1971, lilisaidiwa na Serikali ya China meli 13, rada na wataalamu wetu kupatiwa nafasi mbalimbali za mafunzo...meli hizi zitatuongezea ulinzi katika mipaka yetu majini.

"Kilio kikubwa cha jeshi letu kilikuwa uwezo mdogo wa meli zetu, tumekuwa na kazi ya kutafuta meli hizo na sasa tuna mpango wa kuchukua meli nyingine kubwa zaidi zenye uwezo, kilichobaki ni taratibu za kifedha tu," alisema Rais Kikwete.

Aliongeza kuwa, lazima Tanzania ijenge uwezo wa kulinda mali zetu, mipaka, samaki na mitambo ya gesi ambayo imesimikwa baharini hivi karibuni.

Kwa upande wake, Waziri wa Ulinzi, Dkt. Hussen Mwinyi, alisema Serikali ya China imekuwa msaada mkubwa kwa Tanzania.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange, alisema jeshi hilo limepiga hatua katika ununuzi wa dhana za kivita na kuendeleza mafunzo ya kijeshi.
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akikagua mara baada ya kuzindua rasmi meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam jana April 28, 2015
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akipata picha ya kumbukumbu na makamanda wa meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam jana April 28, 2015
Amiri Jeshi Mkuu Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Chifu Edward Wanzagi wa kabila la Wazanaki (kati) pamoja na Mbunge wa Afrika Mashariki Mhe Makongoro Nyerere baada ya kuzindua rasmi meli vita mbili za doria bahari kuu TNS Msoga na TNS Mwitongo kwenye sherehe zilizofanyika Kamandi ya Jeshi la Maji Kigamboni jijini Dar es salaam jana April 28, 2015.
 
(PICHA NA IKULU)

Muswada wa Sheria ya Mtandao 2015 : Ikulu Yasema Hauna Tatizo Lolote.......Yaweka Wazi Kuwa Rais Kikwete Atausaini


Ikulu imesema Rais Jakaya Kikwete atasaini Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, kwa kuwa umepitia taratibu zote. Pia, Ikulu imesisitiza kuwa sheria hiyo ni nzuri na itadhibiti matumizi mabaya ya mtandao.
 
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alitoa taarifa hiyo jana, alipozungumza na waandishi wa habari, Ikulu jijini Dar es Salaam. Rweyemamu alisema sheria ya Makosa ya Mtandao itasainiwa na rais muda wowote.
 
“Hii ni sheria nzuri, kwanza inadhibiti matumizi mabaya ya mitandao, wote watakaohusishwa ama kutuma au kutumiwa vitu au picha mbaya sheria itawabana wote, na kama umetumiwa bila idhini yako, toa taarifa polisi, ili uwe kwenye upande salama,” alisema Rweyemamu.
 
Alisema madai ya wadau kwamba inanyima uhuru wa kupata taarifa, hayako sahihi kwa kuwa hiyo si sheria ya habari.
 
Alisema kutokuwa na sheria hiyo, si jambo jema kwa usalama wa nchi.
 
Muswada wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ulipitishwa katika mkutano wa 19 wa Bunge, uliofanyika Dodoma hivi karibuni. 
 
Katika mjadala, wabunge wengi walikemea vitendo vilivyokithiri vya uhalifu wa mtandao nchini, na kutaka sheria hiyo itakaposainiwa, itumike ipasavyo kudhibiti.
 
Wabunge wengi walisema viongozi, watu maarufu na jamii kwa ujumla, wamekuwa waathirika wakubwa wa matumizi hayo mabaya ya mtandao, kutokana na kutukanwa, kutishiwa kuuawa, kuzushiwa uongo na hata wakati mwingine kutapeliwa.
 
Hata hivyo, baada ya kupitishwa muswada huo, kumekuwapo na kauli za ukosoaji kutoka kwa watu binafsi na makundi mbalimbali, wakitaka rais asisaini hadi baadhi ya vifungu virekebishwe.
 
Miongoni mwa mambo yaliyokosolewa ni pamoja na sheria kubana pia mtu anayetumiwa vitu au picha mbaya . Wakati huo huo, Rweyemamu akizungumzia Muswada wa Sheria ya Takwimu kuhusu maombi ya wadau ya kutaka ziangaliwe pande zote mbili wakati wa kutiwa hatiani, kutokana na kutoa au kuandika takwimu zisizo sahihi. Alisema maombi hayo yatazingatiwa.
 
Kuhusu Muswada wa Sheria ya Habari, uliopelekwa pia katika mkutano wa Bunge uliomalizika hivi karibuni, Rweyemamu alisema;
 
 “Mimi naomba wadau wa habari wauunge mkono muswada huu, madai kuwa umepelekwa bungeni chini ya hati ya dharura sio kosa, na pia madai kuwa haujajadiliwa na wadau nalo sio sahihi, kwani muswada huu umejadiliwa zaidi ya miaka 10, na mimi pia nilishiriki kwenye moja ya mkutano wa wadau kuujadili miaka hiyo pale Morogoro.”
 
Aidha alisema kuendelea kupinga muswada huo ni kusababisha kuendelea kuwa na sheria ya zamani, jambo ambalo linafanya kukosa sheria mpya. Alisisitiza wadau wa habari kuunga mkono .
 
Ugaidi 
Akizungumzia masuala ya ugaidi, Mkurugenzi huyo wa Mawasiliano Ikulu alishukuru vyombo vya habari kwa kuandika na kuripoti habari za ugaidi kwa kuhabarisha wananchi mbinu za kujihami, iwapo tukio hilo litatokea.
 
Aliomba viendelee kuhabarisha umma taarifa za kujenga na kujihami dhidi ya matukio hayo, bila kuongeza chumvi na ushabiki.
 
“Navishukuru vyombo vya habari vimefanya kazi yao ya kuhabarisha umma kuhusu masuala ya ugaidi na mbinu za kujihami, ila kuna baadhi wamekuwa wakiandika habari hizo kwa ushabiki na kuongeza chumvi, jambo ambalo siyo zuri,” alisema.

Askofu Pengo: Nasumbuliwa na uti wa mgongo, Watanzania Chagueni Rais Masikini


Hatimaye Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo amewatoa hofu Watanzania kuhusu afya yake kwa kueleza kuwa anaendelea vizuri baada ya kufanyiwa uchunguzi wa matatizo yake ya uti wa mgongo.
 
Kardinali Pengo pia amegusia nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu ujao kwa kuwataka watanzania kumchagua rais fukara kuliko anayetafuta nafasi hiyo kwa rushwa.
 
Alitoa kauli hiyo katika mahafali ya Saba ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Joseph, Dar es Salaam jana.
 
Alisema maradhi ya uti wa mgongo ambayo yamekuwa yakimsumbua kila yaligundulika Agosti mwaka 2013 baada ya kufanyiwa uchunguzi wa afya, Ujerumani.
 
“Hospitali ya Ujerumani ndiyo waligundua kuwa nyuzi mbili ndani ya uti wa mgongo zimechanika zinabana mashipa ya neva, kwa hiyo zikawa zinanisababishia maumivu ya mgongo.
 
“Kule Ujerumani walizirudisha katika nafasi yake lakini kwa bahati mbaya hawakufunga huku wakitegemea kuwa mambo yatakwenda vizuri kwa njia ya kawaida.
 
“Lakini kwa sababu ya kurukaruka nikajiona kama nimepona ila baada ya muda kidogo maumivu yasio ya kawaida yalirudi tena,” alisema kiongozi huyo wa kiroho.
 
Alisema maumivu yalipozidi Juni mwaka jana alisafiri kwenda Hospitali ya Manipal, Bangalore, India kwa uchunguzi zaidi.
 
“Walinihudumia vizuri na kwa sasa naendelea vizuri … kwa wale wanaojali uhai wangu nilipokwenda mara ya mwisho kwenye uchunguzi waliniambia kila kitu kimekaa kwenye nafasi yake.
 
“Madaktari walinielezea kuwa nisishangae maumivu ya mara kwa mara kwa sababu operesheni ilikuwa kubwa.
 
“Kwa sababu operesheni ya sasa itachukua muda kati ya miaka miwili hadi mitatu niweze kujisikia mzima kabisa. Kwa sasa naendelea vizuri sina tatizo zaidi,” alisema.
 
Kuhusu Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, Kardinali Pengo alisema ni kitu kibaya kama viongozi wanaowania nafasi ya urais wanatoa rushwa.
 
“Uongozi wa Taifa hauwezi kununuliwa kwa gharama yoyote… wanaoelekea kutoa rushwa baadaye watataka sisi wananchi tulipe zile gharama ambazo walikuwa wametugawia katika kutoa rushwa, afadhali waache kabisa.
 
“Ni vizuri tupate rais anayekuwa fukara lakini anayependa nchi yetu na hatatudai gharama ya kumchangua kama si hivyo gharama inaweza kuwa kubwa ikatusababishia matatizo,” alisema.
 
Kardinali Pengo pia alizungumzia matukio ya ugaidi na kuwataka wanaosambaza ujumbe fupi wa vitisho kuacha mara moja tabia hiyo kwa vile inawaweka wananchi katika hofu.
 
“Wanaweza kusababisha taharuki na mikanganyiko na kuleta madhara kwa wengi kwa kitu ambacho hakipo.
 
“Kama kuna hofu ya usalama sehemu yoyote inabidi tuwaachie wataalamu wa usalama waweze kuishughulikia kwa namna wajuavyo,” alisema.
 
Hata hivyo, aliitaka serikali kupitia Idara ya Usalama kuwa ya kwanza kuwahakikishia wananchi kuwa hakuna matukio hayo amani na utulivu viendelee kuwapo.
 
Pia aliwashauri wahitimu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Josesph kuwa wasisome kwa ajili ya kuajiriwa na serikali tu.
 
“Kuna nafasi za wataalamu wa sayasi na sanaa za kujiajiri katika chuo hiki … Chuo kikuu kizuri ni kile kinachoandaa wanafunzi kujiajiri,” alisema.
 
Mkuu wa Chuo hicho, Padre Aru Raji alisema chuo kinazidi kupanuka na mwaka huu kinatarajia kufungua Chuo Kikuu Sumbawanga na Chuo cha Afya na Tiba, Boko, Dar es Salaam.

Breaking News:Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Yaahirisha Kura ya Maoni Ya Katiba Mpya


Tume ya Taifa ya uchaguzi (NEC) imesema kuwa kura ya maoni ya katiba inayopendekezwa, haitaweza kufanyika tena tarehe 30 April hadi hapo itakapotangazwa tarehe nyingine tena.
 
Katika kikao chak  na   waandishi  wa  habari  leo  mchana,NEC imesema sababu ya kuhairisha kura hiyo April 30 ni kutokana na kutokamilika kwa zoezi la uboreshaji daftari la kudumu la wapiga kura.

IGP Mangu Afanya Mabadiliko Kwa Baadhi ya Makamanda wa Polisi wa Mikoa.


Inspekta Jenerali wa Polisi IGP Ernest Mangu amefanya mabadiliko kwa baadhi ya makamanda wa polisi wa mikoa.

Miongoni mwa makamanda wa mikoa waliofanyiwa mabadiliko ni pamoja na aliyekuwa kamanda wa Mkoa wa Simiyu, Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Charles Mkumbo anakwenda kuwa kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa afisa mnadhimu mkoa wa Manyara Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Gemini Mushi.
 
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Valentino Mlowola anakwenda kuwa Kaimu Kamishna wa Intelijensia makao makuu. 
 
Aliyekuwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Maria Nzuki amehamishwa makao makuu kuwa mkuu wa polisi jamii na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa kamanda wa kikosi cha ufundi Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Lucas Mkondya.

Wengine ni aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kilimanjaro Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Godfrey Kamwela amehamishiwa Polisi Makao Makuu na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Njombe Kamishna Msaidi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Fulgence Ngonjani.
 
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei amehamishiwa Kanda Maalum ya Dar es Salaam kuwa mkuu wa utawala na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Jafary Mohamed.
 
Aidha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ferdinand Mtui aliyekuwa mkuu wa operesheni maalum polisi makao makuu ameenda kuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Kigoma.

Zaidi ya hao wengine waliyohamishwa ni pamoja na aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Frasser Kashai amehamishiwa Polisi makao makuu na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa mkuu wa upelelezi mkoa wa Iringa Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Zuberi Mwombeji.
 
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Temeke Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Kihenya Kihenya amehamishiwa polisi makao makuu na nafasi yake kuchukuliwa na aliyekuwa mkuu wa polisi wa wilaya ya kati Ilala, Dar es Salaam Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Andrew Satta.

Kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Jeshi la Polisi, mabadiliko hayo ni ya kawaida katika kuhakikisha kwamba usalama wa raia na mali zao unaendelea kuimarika.

Imetolewa na:
Advera Bulimba-SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.

Wazazi 19 Wahukumiwa Kwa Kushindwa Kupeleka Watoto wao Shule


Wazazi 19 wa wanafunzi walioshindwa kuripoti kidato cha kwanza kwa mwaka wa masomo wa 2014/2015 wamehukumiwa kifungo cha nje cha miezi mitatu kila mmoja kutokana na kosa la kushindwa kuwapeleka watoto wao shuleni.
 
Wazazi waliohukumiwa kifungo hiki ni wale wa kata za Mpindimbi na Lukuledi zilizopo katika Halmashauri ya wilaya ya Masasi, Mtwara .
 
Aidha, wametakiwa kuripoti kwenye Mahakama ya Mwanzo ya Lisekese wilayani hapa kila baada ya wiki mbili wakati wote watakapokuwa wanatumikia adhabu yao.
 
Mbele ya Hakimu wa Mahakama ya Mwanzo ya Lisekese wilayani Masasi, Gloria Mkwera karani wa mahakama hiyo, Agnes Hanga alidai washitakiwa hao walitenda kosa hilo mwanzoni mwa mwaka huu  waliposhindwa kutimiza wajibu wao wa kuwapeleka watoto wao shuleni huku wakijua ni wajibu wao.

Breaking News: Mwenyekiti wa Jumuia ya Wafanyabiasha Nchini Aaachiwa Kwa Dhamana


Habari  Zilizotufikia  zinadai kuwa Mwenyekiti wa Jumuia ya wafanyabiasha nchini Tanzania Bwana Jonson Minja ameachiwa kwa dhamana na Mahakama ya Hakimu mkazi Mkoa wa Dodoma baada ya wafanyabiashara kuweka mgomo ambao ulikuwa haujafahamika ukomo wake.
 
Sakata  hili la wafanyabiashara kufanya mgomo wa kufunga maduka katika mikoa mbalimbali nchini,  jana lilichafua hali ya hewa bungeni baada ya baadhi ya wabunge kuitaka Serikali itoe tamko kuhusu hali hiyo.

Tukio hilo liliibuka bungeni Mjini Dodoma jana baada ya  kipindi cha maswali na majibu ambapo wabunge waliomba  mwongozo ili kuhoji hali inayoendelea nchini dhidi ya baadhi ya wafanyabiashara kufunga maduka.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda na Biashara ambaye pia ni Mbunge wa Kisesa, Wilaya ya Meatu, mkoani Simiyu, Luhaga Mpina, alishangazwa na  kauli zinazotolewa na Serikali kuwa mambo yao na wafanyabiashara yako sawa badala ya kueleza walichojadili na kufikia makubaliano.

"Waziri wa Fedha (Saada Mkuya), amekuwa akihudhuria katika vikao hivyo, kusikiliza hoja zao hivyo tunachokitaka alieleze Bunge hili suala linaloendelea si kusema uongo.

"Mwaka 2014 Serikali iliunda Kamati ya Maridhiano ambayo ilishirikisha wafanyabiashara waweze kukaa pamoja na Serikali kujadili na kufikia mwafaka lakini imechukua muda mrefu kuitisha  vikao ili kujadili kwa pamoja,"
alisema.

Alisema hata wakiitisha vikao hivyo, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara hao hayupo; hivyo itakuwa kazi bure na
kuitaka Serikali iangalie namna ya kumpatia dhamana kiongozi huyo ili vikao hivyo viendelee.
 
Mwenyekiti huyo anakabiliwa  na mashtaka mawili ya kuwachochea wafanyabiashara mkoani Dodoma kutenda kosa na kuwakataza wafanyabiashara nchini wasitumie mashine za kieletroniki za kukusanya kodi za EFDS ambavyo vyote ni makosa ya jinai.
 
Endelea kuwa  nasi  kwa  habari  motomoto.

Muswada wa Mahakama ya Kadhi Waondolewa.....Hautawasilishwa Bungeni LEO.


Muswada wa Mahakama ya Kadhi umeondolewa bungeni na sasa hautajadiliwa katika Mkutano wa 19 wa Bunge unaohitimishwa leo mjini  Dodoma.

Huu ni muswada wa tatu kuondolewa Bungeni baada ya ile miwili ya sekta ya habari ambayo ni muswada wa Sheria ya kupata Taarifa wa mwaka 2015 na ule wa sheria ya huduma wa Vyombo vya Habari iliyoondelewa mwishoni mwa wiki iliyopita.

Muswada huo ulipangwa kuwasilishwa Bungeni leo, lakini serikali imeamua kuuondoa kutokana na hofu ya kutokea mpasuko nchini.

Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila, akizungumza na mwandishi wetu jana ofisini kwake alisema muswada wa Mahakama ya Kadhi hautakuwapo tena katika mkutano huo.

Dk. Kashilila alisema haijulikani ni lini utawasilishwa bungeni kwa sababu Mkutano wa Bunge ujao unaotarajia kufanyika Mei, utakuwa mahsusi kwa ajili ya bajeti.

“Waziri Mkuu alivyosema wataangalia na kushauriana kimsingi, alitoa maneno ya busara tu au ilikuwa kauli ya mtu mzima, lakini huu muswada hautakuwapo,” alisema.

Dk. Kashilila alisema hali iliyojitokeza Jumapili iliyopita wakati wa semina ya wabunge haikuwa nzuri kutokana na mvutano mkali miongoni mwa wabunge.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, George Masaju, alipoulizwa kuhusu kama muswada huo utawasilishwa bungeni, alisema hakuwa na majibu badala yake alitaka suala hilo iulizwe ofisi ya Spika.

“Suala hili usiniulize, nenda Ofisi ya Spika au muulize huyu (Magati) ambaye yupo sekretarieti,” alisema huku akiwa na haraka kuelekea ofisini kwake.

Naibu Spika, Job Ndugai, akizungumza na mwandishi  nje ya ukumbi wa Bunge muda mfupi baada ya kuahirisha Bunge, alisema muswada wa Mahakama ya Kadhi hautawasilishwa bungeni leo.

“Huo muswada hauwezi kuletwa bungeni kutokana na hali ilivyo,” alisema Ndugai bila kufafanua zaidi.

Naye Waziri wa Sheria na Katiba, Dk. Asha-Rose Migiro, alipoulizwa kama muswada huo utawasilishwa bungeni alimtaka mwandishi asimuulize maswali yanayohusiana na muswada wa Mahakama ya Kadhi.

“Sitaki kabisa kuulizwa suala la Muswada wa Mahakama ya Kadhi, “alijibu Dk. Migiro kwa hasira huku akiingia kantini.

Tujikumbushe
Februari mwaka huu, muswada huo pia uliondolewa bungeni kwa kile Mwanasheria Mkuu wa Serikali alichodai kwamba ni kwenda kuonana na viongozi wa dini kuwaelemisha juu ya mahakama hiyo, ili uwasilishwe tena kwenye mkutano unamalizika leo.

Mwishoni mwa wiki nusura wabunge wazipige kavu kavu huku wakirushiana maneno wakati wa semina kuhusu Mahakama ya Kadhi.
 
 Kutokana na joto lilivyopanda, baadhi waliamua kususia semina hiyo na kutoka huku wengine wakibaki na kurushiana vijembe. Semina hiyo iliandaliwa na Bunge.
Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top