Habari Kali
Loading...

Interview na Akothee, Mkenya mwingine aliyefanya kolabo na Diamond Platnumz

Akothee amekua msanii wa kwanza Kenya kufanya kolabo na mwimbaji Mtanzania Diamond Platnumz, ni Mwanamke mwenye historia ndefu ya maisha ya kuanzia kuwa Dereva Taxi Mombasa Kenya kabla hajaolewa na Mzungu na kwenda Ulaya kisha baadae akarudi Kenya baada ya ndoa kuvunjika.
Anasema ‘Mimi huwa napenda raha sana, kuna wakati Diamond alikuja Mombasa mwaka 2013 ambapo nilikua miongoni mwa watu waliokwenda kuchukua watu wake Airport nikajiuliza kwanini siku moja nisifanye wimbo na huyu kijana wa bongo? kweli nimefanikiwa kurekodi naye hatimaye, siwezi kusema kama Diamond kanitoza pesa kurekodi naye ila ngoma imechukua gharama kubwa’
Tazama hii video hapa chini akijieleza zaidi kisha video ya wimbo wenyewe chini ya hii video.

Diamond atoa sababu ya kukacha All White Party ya Zari, adai hamwogopi Ivan


Diamond Platnumz alikuwepo, Kampala, Uganda usiku ambao Zari alikuwa akifanya party yake ya All White lakini hakutokea. Ex wa Zari, Ivan Ssemwanga na wapambe wake walikuwepo. 
 
Watu walihisi kuwa Diamond aliogopa kwenda kumpa kampani mama wa mtoto wake Tiffah ili kuepusha shari na kambi ya Rich Gang ya Ivan.

Hata hivyo muimbaji huyo wa Utanipenda amedai kuwa hakukacha party hiyo bali makubaliano aliyokuwa nayo na promota wa show yake ya Ijumaa (siku moja baada ya all white party) yalimtaka asiende kwenye show hiyo ili kutengeneza uspesho kwenye show yake na Patoranking na sio ukweli kuwa alimgwaya Ivan.
 
“Halafu sasa watu wanasema namuogoa [Ivan], mimi siwezi kumuogopa, hii code chafu kabisa kutoka Tandale mimi nimuogope mtu!,” alisema kwenye mahojiano ya jana kwenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM.
 
Diamond amesema ameshawahi kukutana na Ivan mara kibao japo walipigiana mikausho kama kawa!
 
“Sijawahi kuwa na matatizo naye, nshakutana naye wakati naenda kwenye MTV alikuwepo, mara nyingi tulikuwa tunapishana hivi na hivi kabisa. Hatujawahi kusalimiana sababu sijawahi kuwa na mahusiano naye niseme nimsalimie ni uongo. Halafu nilikuwa nikipita, nipo na crew, security, yeye anakuwa anapita tu maskini ya Mungu.”
Mpekuzi blog

MISS TZ AMCHOKONOA ZARI KWA DIAMOND!


Musa mateja
Madai mazito! Mshiriki wa Kinyang’anyiro cha Miss Tanzania 2011/12 ambaye alianza harakati za kunyakua taji hilo akitokea Mkoa wa Shinyanga na baadaye kutwaa Taji la Miss Kanda ya Ziwa, Glory Samwel anadaiwa kumchokonoa Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwa kile kinachodaiwa kuwa ana ukaribu wa ‘kimalovee’ na mpenzi wa Zari, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa katika pozi na miss huyo.
Chanzo cha ‘unyunyuzi’ huo kilitonya kwamba, mlimbwende huyo amekuwa akionekana mara kwa mara akijivinjari na Diamond jambo ambalo wadau wamelishtukia na kubaini kuwa ana mpango wa kuingilia penzi la Zari na kusambaratishia uchumba wa wawili hao.
Ijumaa Wikienda lilinyetishiwa habari hizo hivi karibuni na kuamua kuzifanyia kazi hatua kwa hatua, ambapo liliweza kujiridhisha kwa baadhi ya matukio ya picha ambazo mrembo huyo amekuwa akipiga na Diamond.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Mbali na picha pia kuna matukio ya sherehe za ‘bethidei’ ambazo Diamond alionekana akiwa karibu na mrembo huyo.
Ukiachilia mbali uchunguzi huo, mwanahabari wetu alimtafuta mrembo huyo kwa lengo la kutaka kujiridhisha juu ya madai hayo ambapo alikiri kuwa na ukaribu na Diamond huku akifafanua kwamba uhusiano wake na jamaa huyo si wa kimapenzi kama wengi wanavyomchukulia.
“Hizo picha za karibu zaidi ni zile ambazo tulipiga kwenye bethidei ya meneja wa Diamond aitwaye Salaam, ambayo ilifanyika pale nyumbani kwake (Salaam) Kijitonyama (Dar) hivi karibuni.
“Ni kweli watu wengi wananituhumu kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Diamond lakini si kweli maana ninajuana naye kawaida tu,” alisema Glory.
Kwa upande wa Diamond aliliambia Ijumaa Wikienda kuwa ni kweli anamfahamu Glory ila si mpenzi wake na anachokijua ni shabiki wake kama ilivyo kwa wengine.
Alisema hata picha alizopiga naye hakuna picha za hovyo maana zilipigwa hadharani.
“Glory ni shabiki wangu wa kawaida tu kama ilivyo kwa mashabiki wangu wengine, suala la kupiga naye picha halimaanishi ni demu wangu,” alisema Diamond.

DIAMOND: TAYARI NIMEMVALISHA PETE YA UCHUMBA ZARI, KUINGIA KATIKA NDOA MWAKA HUU

Diamond na mpenzi wake Zari katika Exclusive One on One Interview ya Power Breakfast ya Clouds FM na 360 ya Clouds TV.
STAA wa Bongo Fleva nchini, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' amefunguka kuwa tayari amemvalisha pete ya uchumba mpenzi wake Zarinah Hassan 'Zari' na anatarajia kupata mtoto wa kike mwaka huu.
Diamond ameyaongea hayo hivi punde katika Exclusive One on One Interview ya Power Breakfast ya Clouds FM na 360 ya Clouds TV kuelekea katika shoo ya Zari All White Party itakayofanyika leo usiku katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar.
Katika mahojiano hayo ambayo Diamond ameambatana na mpenzi wake huyo, ameongeza kuwa anatarajia kuingia katika ndoa mwaka huu.
Kwa upande wa Zari yeye amefunguka kuwa bado hajajua jina watakalompa mtoto wao wa kike anayetarajiwa kuzaliwa mwaka huu ila watampatia jina zuri la Kiislam na lenye mvuto.

DIAMOND, ZARI WAFANYIWA EXCLUSIVE INTERVIEW CLOUDS TV/RADIO

Diamond na mpenzi wake Zari katika Exclusive One on One Interview ya Power Breakfast ya Clouds FM na 360 ya Clouds TV.
Diamond akimuweka sawa mpenzi wake.
Mtangazani mwenye jina kubwa wa Radio Clouds FM, Gerald Hando 'Mzee Mnoko' (kushoto) na Edson Kamoga wa 360 ya Clouds TV (kulia) wakiendelea kufanyia mahojiano Diamond na Zari.
Mtangazaji wa Clouds FM, Millard Ayo akisoma meseji za mashabiki waliokuwa wakifuatilia mahojiano hayo.
Baadhi ya wadau wa Clouds TV, Radio (kulia) wakipata kifungua kinywa kilichokuwa kimeandaliwa.
P Diamond na Zari wakiwa katika pozi na wadau wa Clouds TV, Radio baada ya mahojiano.
Wakati wakitoka.
Wadau wakiwa kwenye gari la Diamond wakati akijiandaa kuondoka mahali hapo.
(PICHA: MUSA MATEJA/GPL)

SHOO YA ZARI ALL WHITE PARTY YANUKIA, DIAMOND AJIPINDA KUHAKIKI TIKETI


STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond' jana ametupia picha hii mitandaoni akihakiki tiketi kwa ajili ya shoo ya mpenzi wake Zarinah Hassan 'Zari' ya ZARI ALL WHITE PARTY itakayofanyika Ijumaa ya Mei 1, mwaka huu kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar.
Staa huyo aliisindikiza picha hiyo kwa maneno haya:
"Sio kwa kiingilio hiki cha kuanzia Elf 50 hadi Milioni 3 eti nikajifanya naleta Uboss ... Mzigo Nausimamia mwenyeweee!!! Kushoto Manager @salaam_sk katikati nna @juju_utamu huku @queendarleen4real halaf kwambaaaaaali Mtoto katulia zake Anachat chat!... HAYA WALE WA ELFU HAMSINI NA WA LAKI KESHO NTAWATAJIA VITUO ZITAPOPATIKANA TICKET!!! #ZARIALLWHITEPARTY Friday May 1st 2015 Mlimani City Dar!!"
Kwenye shoo hiyo ya Zari, watu mbalimbali mashuhuri wanatarajiwa kuhudhuria akiwemo dairekta mkubwa Afrika, Godfather wa Afrika Kusini na Top Ten ya Washiriki wa Shindano la Big Brother ‘Hot Shot’ 2014.

ZARI AZUIWA KUJIFUNGULIA A. KUSINI


Imelda Mtema
Stop! Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amemzuia mama kijacho wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwenda kujifungulia nje ya Bongo pindi mambo yatakapokuwa tayari.
                             Mama kijacho wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
Habari zilizonyakwa na Ijumaa Wikienda kutoka kwenye chanzo cha ndani ya familia ya Diamond zilieleza kwamba, tayari jamaa huyo amemuanzishia Zari kliniki Bongo.
Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na mama kijacho wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
“Yaani Diamond hataki kabisa Zari kwenda kujifungulia South Africa (Sauzi). Anataka kila kitu kifanyike hapahapa Bongo. Tayari amemuanzishia kliniki kwenye Hospitali ya AMI (ipo Masaki, Dar),” kilitonya chanzo hicho.
Akizungumzia ishu hiyo, Diamond alisema kuwa anatamani kuwa karibu na mama kijacho wake huyo hivyo ni kweli anataka mwanadada huyo ajifungulie Bongo.

Diamond au Baba Kijacho alisema lengo la kufanya hivyo ni ili iwe shangwe kwa familia nzima tofauti na atakapojifungulia nje ambapo familia italazimika kusafiri kwenda kumuona Chibu Junior.
Kwa mujibu wa Diamond, Zari ambaye ni mama wa watoto watatu akifukuzia huyo wa nne anatarajia kujifungua kati ya mwezi Julai au Agosti, mwaka huu.

KAMA ULIKUWA UNADHANI UJAUZITO WA ZARI NI FEKI, TAZAMA HII PICHA AKIONYESHA MIMBA ILIVYOKUA KUBWA!



Zari 2 
Labda uliziona picha za mwanzoni za mrembo Zari kutoka Uganda lakini ukaamini maneno ya wengine kwamba shemeji yetu huyu kwa Diamond Platnumz alidanganya kuhusu kuwa na ujauzito huo wa Diamond.
Picha mpya kutoka kwake right now ni hii hapa chini ikionyesha jinsi ujauzito wake unavyozidi kukua…
Zari 1

ZARI AZUA KIZAAZAA MSIBANI

Dustan Shekidele, Morogoro
Kazi ipo! Mwandani wa staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari’ juzikati alizua kizaazaa kisa ujauzito alipohudhuria kwenye msiba wa aliyekuwa bosi wa Tip Top Connection, Abdul Taletale ‘Abdul Bonge’ aliyefariki dunia ghafla wikiendi iliyopita.
Mwandani wa staa mkubwa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari akifichwa na bodigadi wake.
Tukio hilo la Zari lilichukua nafasi katika Kijiji cha Mkuyuni, Tarafa ya Matombo mkoani hapa ambapo mastaa kibao walisafiri kutoka Dar kwa ajili ya mazishi ya kiongozi huyo.
ILIKUWAJE?
Awali, katika tukio hilo lililoshuhudiwa na Ijumaa mapema Jumanne wiki hii, Zari na Diamond, wakiwa wameongozana na wapambe wao walifika eneo la msiba ambapo kwa taratibu za Kiislam, wanawake hawachanganyiki na wanaume hivyo Zari akachukuliwa kwenda upande mwingine huku Diamond akielekea upande wa wanaume.
HALI YA HEWA YABADILIKA
Mara baada ya mastaa hao kutinga eneo hilo, umati mkubwa uliokuwa msibani hapo ulianza kuwazingira huku kila mmoja akitaka kuwaona.Akiingizwa garini.
ZARI AIBUA KIZAAZAA
Akiwa upande wa wanawake wenzake, Zari alijikuta akizungukwa na baadhi ya watu walionekana wazi kumchunguza kuanzia miguuni hadi kichwani ikidaiwa kuwa, walikuwa wakicheki kama kweli ana mimba ya Diamond.
“Mwee, huyu ndiye Zari wa Diamond! Hivi mimba anayo kweli au ndiyo haya mambo ya mastaa wetu, mhh lakini kweli kitumbo kama kimetuna vile,” alisikika akisema mmoja wa wanawake hao.Uwepo wa mwanadada huyo uliwafanya wengi kusahau ishu ya msiba na kujikuta wakipigana vikumbo kumshangaa Zari ambaye muda mwingi alikuwa akijificha.
Kutokana na mazingira ya watu kukanyagana kutaka kumuona staa huyo, mrembo aliyefahamika kwa jina la Jestina George aligeuka kuwa bodigadi wake ili kumuepushia usumbufu ambapo alifanya kazi ya kumlinda.
PAPARAZI AZUIWA KUMPIGA PICHA
Paparazi wetu aliyekuwa eneo la msiba kwa lengo la kupata picha za kumbukumbu kwamba Zari aliwahi kufika eneo hilo, alikumbana na wakati mgumu baada ya Jestina kumpiga mkwara asijaribu kupiga picha.
 “Weee, ukijaribu kupiga picha tunakorofishana, mwenyewe hataki kupiga picha, kama vipi nenda kamuombe ruhusa Diamond,” alisema Jestina huku akimficha Zari.Diamond akiimalisha usalama kwa mpenzi wake.
WATU WAANZA ZOGO
Kufuatia kitendo cha Jestina kumzuia mwandishi wetu kupiga picha, zogo lilianza eneo hilo huku baadhi ya watu wakihoji sababu za Zari kufichwa.“Au ni hiyo mimba yake ndiyo maana hamtaki apigwe picha? Acheni hizo bwana,” alisikika akiwaka kijana mmoja.
PAPARAZI AMFUATA DIAMOND
Baada ya paparazi kupigwa mkwara asipige picha alilazimika kwenda kumtafuta Diamond ili ampe ruhusa ya kwenda kumfotoa Zari lakini staa huyo naye alikataa na kueleza kuwa, kama anataka kufanya hivyo akachukue ruhusa kutoka kwa meneja wake.
Meneje huyo wa Diamond aliyefahamika kwa jina moja la Salam alipofuatwa alimruhusu paparazi kufanya kazi yake lakini aliporudi nyumbani palipokuwa na msiba kwa nia ya kumfotoa Zari, hali ilikuwa ileile hivyo kumsubiria mpaka Diamond alipotoka makaburini na alipofika kwenye gari lao, Zari alitolewa kwa kufichwa na Jestina kiasi cha kuwepo ugumu kupata sura yake.
ZARI AINGIA KWENYE GARI FASTA
Huku watu wakimfuata kwa nyuma, Jestina alimchukua Zari na kumficha kwapani kisha kumkimbizia kwenye gari tayari kwa kuondoka eneo hilo.
DIAMOND NAYE APATA WAKATI MGUMU
Wakati Diamond akirejea kutoka makaburini, alijikuta akizingirwa na baadhi ya vijana ambao wengi wao hawajawahi kumuona ‘live’ hivyo kumpa wakati mgumu.Hata hivyo, ili kuwafurahisha, vijana hao walipata fursa ya kupiga naye stori mbili-tatu kabla ya kuondoka eneo hilo na kuacha umati ukiwasindikiza kwa macho.

BABA DIAMOND AMFAGILIA ZARI

Kukubali! Baba mzazi wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Jumaa ‘Baba D’ amefunguka kuwa, kwenye listi ya wanawake wote waliowahi kuwa na mwanaye kimalovee, mwanadada Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ ndiye mkwe wa ukweli kwake kutokana na kuwa tayari kumletea mjukuu.
Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mpenzi wake Zarinah Hassan 'Zari'.
Akizungumza na Amani, juzikati jijini Dar, baba Diamond alisema kuwa miongoni mwa vitu ambavyo vilikuwa vikimkosesha amani ni maneno yaliyokuwa yakimsakama Diamond kuwa huenda hana uwezo wa kumpa mimba mwanamke, kiasi cha warembo wote aliowahi kuripotiwa kutoka nao kutoka patupu bila kushika ujauzito.
“Nawashangaa sana hao wanawake si huyo Wema (Sepetu) wala hao wenziye, maana Diamond alisema kampa mimba Penny (Penniel Mungilwa) zikatoka huku mwenyewe akikanusha hajawahi kushika mimba kwa kumchafua tu mwanangu aonekane siyo mwanaume rijali,” alisema mzazi huyo.
Baba mzazi wa mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Abdul Jumaa ‘Baba D’.
Baba D alitiririka kwamba mastaa hao wa kike ambao Mbongo Fleva huyo aliwahi kutoka nao huenda wao ndiyo hawana kizazi hivyo wanamtupia lawama mtoto wake kwa kushindwa kuwazalisha.
Alisema kuwa kikubwa anachokiamini wote hawakuwa na upendo wa kweli kwa mwanaye, walitaka kuzitumia tu fedha zake na kumuacha solemba lakini sasa Zari ndiye mwenye penzi la dhati kwa mwanaye.
“Kiukweli Zari kanifurahisha. Ndiye mkwe wangu wa kweli na halali kabisa.
“Nampongeza sana Zari kwa kushika ujauzito wa mwanangu. Sasa Diamond atatembea kifua mbele kwa kujiamini,” alisema baba D.
Alisema kutokana na kile kilichokuwa kikiaminika kuwa hana maelewano mazuri na mkali huyo wa Bongo Fleva, kwa sasa wapo vizuri na hata akiwa na tatizo huwa anamwambia Diamond ambaye amekuwa akimpa msaada.
“Kwa sasa nina maelewano mazuri na Diamond, muda wowote nikiwa na tatizo huwa namjulisha ananisaidia, kitu ambacho kinamfanya amgharamie mama yake kuliko mimi ni kwa sababu aliishi naye kwa kipindi kirefu na kuhangaika naye tangu utotoni,” alisema.
Ukiacha Zari ambaye amekubali kubeba ujauzito wake, Diamond aliwahi kuwalalamikia baadhi ya wapenzi wake kuwa walikataa kumzalia mtoto akiwemo Wema, Penny na Jokate Mwegelo.

"Mimba My Foot"... Mashabiki wa Zari (Mpenzi wa Diamond ) Wamvaa Wema Sepetu baada ya kukejeli Mimba Yake


Wema Sepetu anahisi ujauzito wa Zari The Boss Lady ni geresha tu, hakuna lolote!

Hii ni kwa mujibu wa picha inayoonekana kuwa iliwekwa kwenye ukurasa wa Instagram wa Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 na ex wa Diamond Platnumz.
 
Picha hiyo haipo tena lakini Zari alifanikiwa kuipata na kuiweka kwenye ukurasa wake  wa  pili (zarithebosslady_) kuelezea alivyosikitishwa na kauli ya Wema kwenye picha yake (Zari) isemayo ‘mimba my foot’. 
 
Kwa mujibu wa urbandictionary.com msemo ‘my foot’ humaanisha: An exclamation that means that one believes the previous speaker’s statement to be untrue
 
Mrembo huyo wa Uganda anayetarajia kumzalia Diamond mtoto wake wa kwanza, aliipost picha hiyo na kuifuta tena baadaye na kuandika: 

"Astagafululah! May God Protect Zarimond and chibu junior #zaritlale #chibujunior #zarihassan #chibudangote"

Diamond kuachia nyimbo 4 mfululizo kabla ya March, ikiwemo collabo yake na Fally Ipupa



Mwaka jana mwishoni (2014) baada ya Diamond kukutana na wasanii wakubwa wa Afrika wakiwemo Fally Ipupa na P-Square nchini Nigeria, alisema “nikikutana na 18 huwa naachia bonge la shuti mpaka nishinde” na kauli yake imetimia.

Staa huyo wa ‘Ntampata Wapi’ amefanikiwa kufanya collabo na staa wa DRC, Fally Ipupa ambayo ni miongoni mwa nyimbo nne alizopanga kuzitoa kati ya sasa na mwezi wa tatu.
 
Meneja wa Diamond, Babu Tale amesema kuwa wanampango wa kutoa nyimbo nne mfululizo hadi kufika mwezi wa tatu 2015, zikiwemo za Diamond na zingine alizofanya collabo na wasanii wa nje.
 
“Huu mwaka tunaugeuza vizuri kutoka January mpaka March tuna release nyimbo nne mfululizo ambazo ni za Diamond na zingine ni za watu wa nje ambao feauturing Diamond.
 
 Fally ametokea kumkubali Diamond, kwahiyo ngoma inakuwa ya Fally na Diamond, kila mmoja anafanya kwenye sebule yake tunakutana kwenye video kama ni Godfather, kama ni Adam, kama ni Moe Musa kama ni nani yeyote yule” Alisema Babu Tale kupitia Amplifaya ya Clouds Fm.

DIAMOND: PENNY NDIYE MWALIMU WANGU WA KIINGEREZA

Stori: Musa Mateja
WAKATI kila mtu akiamini mwalimu wake wa lugha ya Kiingereza ni Wema Sepetu ‘Madam’ staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameibuka na kudai aliyemfundisha lugha hiyo ni aliyekuwa mpenzi wake, Peniel Mungilwa‘Diamond aliwataka watu wote waliokuwa wakiamini Wema ndiye mwalimu wake wa ung’eng’e wafute imani hiyo kwani Penny ndiye mpango mzima.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ wakati akiwa na 'Penny'.
“Ujue kila mtu huwa ana hisia zake na wengi wamekuwa wakiishi kwa hisia, nimekuwa nikiambiwa kuwa Wema ana mchango mkubwa katika uzungumzaji wangu wa Kiingereza jambo ambalo si kweli, aliyenifundisha lugha hiyo kwa sehemu kubwa ni Penny maana aliniletea hadi mwalimu ingawa nilikuwa nikimlipa mwenyewe,” alisema Diamond.

ZARI, DIAMOND MAHABA KWEUPE UGANDA

STORI: HAMIDA HASSAN na Musa Mateja
STAA anayetamba na ngoma mpya ya Nitampata Wapi, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na mtoto mzuri kutoka Uganda, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wameoneshana malovee hadharani na kuwaacha watu midomo wazi.
Nasibu Abdul ‘Diamond’akiwa kwenye pozi na mtoto mzuri kutoka Uganda, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’.
Tukio hilo lililoacha historia ya aina yake kwa kutokana na umaarufu wa wawili hao, lilitokea Jumatano iliyopita, nchini Uganda wakati Zari alipokwenda kumpokea Diamond katika Uwanja wa Ndege wa Kampala nchini humo.‘Zari The Boss Lady ‘Diamond wakipata ukodaki.
Kwa mujibu wa chanzo kilichoambatana na Diamond, Zari alimpokea mgeni wake kwa mabusu motomoto na msafara wa kwenda hotelini ulipoanza, walipewa ulinzi mzito hadi hotelini ambako kila wakati wawili hao walipeana mabusu ya kiaina kuonesha ‘wamemisiana’.
Alipotafutwa Diamond kwa njia ya simu ya mkononi, hakutaka kufungukia mahaba hayo yaliyozua gumzo zaidi ya kucheka na kusema amejiandaa vilivyo kumpa sapoti Zari katika shoo yake ya All White Part iliyotarajiwa kufanyika juzi nchini humo.“Mwanangu nimejipanga, kitanuka mbaya katika hii shoo si unajua huwa sirudi nyuma?” alisema Diamond.

DIAMOND ATWAA TUZO 3 ZA CHANNEL O SAUZ

Diamond akiwa na tuzo.
MSANII Naseeb Abdul ‘Diamond Platumz’ ametwaa tuzo tatu za Channel O usiku huu nchini Afrika Kusini. Tuzo hizo ni; Most Gifted new comer, Most Gifted Afropop na Most Gifted East kupitia wimbo wake wa Number One!

NASIBU ABDUL ALISHAFANYA VIBARUA ILI APATE FEDHA YA CHAKULA

Na Mwandishi Wetu
ANAITWA Nasibu Abdul au maarufu kwa jina la Diamond. Alizaliwa saa kumi na moja jioni ya Oktoba 2, 1989 katika Hospitali ya Amana iliyopo Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam. Wazazi wake walimpa jina la Nasibu wakiamini ni la bahati.
Mkali wa Bongo fleva, Nasibu Abdul au maarufu kwa jina la Diamond akipozi.
Diamond aliongea hivi karibuni na safu hii ya Mjue Huyu ambapo aliweka wazi mambo mengi ya maisha yake. Diamond akiwa hajapata ufahamu, yaani bado mdogo, wazazi wake walitengana kwa sababu ambazo bado hazijawa wazi na baba yake kumuacha na mama.
WAZAZI WATENGANA, DIAMOND AENDA KWA BIBI
Kufuatia hali hiyo, ilibidi mama yake ahamie kwa mama yake mzazi (bibi wa Diamond), Tandale Magharibi, Dar. Hapo ndipo yakawa makazi ya mama huyo na mwanaye.
Mnamo mwaka 1995, Diamond alianza  elimu ya awali katika Shule ya Chakula Bora iliyopo Tandale- Uzuri. Mwaka 1996 alianza elimu ya msingi katika Shule ya Msingi Tandale- Magharibi iliyopo jijini Dar es Salaam.
DALILI YA KUWA MWANAMUZIKI
Mwaka 2000, Diamond akiwa darasa la tano alianza kupenda muziki, hivyo akawa anakopi baadhi ya nyimbo za wasanii waliokuwa wakihiti ndani na nje ya Bongo na kuimba yeye katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam. Kwa kuliona hilo, mama yake alianza kumnunulia kanda za albamu za wasanii tofauti hata kumwandikia baadhi ya nyimbo za wasanii hao ili mwanae aweze kuzishika na kuimba kirahisi.
ASOMA, APELEKWA KWENYE MATAMASHA
Diamond alizidi kuupenda muziki ikabidi mama yake awe anampeleka kwenye matamasha mbalimbali ili mwanae apate nafasi ya kuimba.
Baadhi ya ndugu walimjia juu mama huyo wakidai anamharibu mtoto badala ya kumuhimiza masomo anamwingiza kwenye muziki ambao walidhani haukuwa na faida yoyote.
MAISHA MAGUMU
“Kusema ukweli pamoja na yote hayo, hali ya maisha ilikuwa si nzuri kwa mama maana hakuwa na kazi ya maana wala vyanzo vikubwa vya fedha, hivyo  ilibidi atumie kiasi kidogo alichokipata kutoka kwenye kodi ya vyumba viwili alivyopewa na bibi ili kunisomesha,” alisema Diamond.
CHUMBA KIMOJA NA MAMA
Diamond aliendelea kusema kuwa, kutokana na kupangisha vyumba viwili ilibidi yeye na mama yake kuhamia kwenye chumba cha bibi yake na maisha yakaendelea humo.
AMALIZA SHULE YA MSINGI
Mwaka 2002, Diamond alimaliza masomo ya elimu ya msingi lakini ili aende sekondari, mama yake alimwambia aachane na habari ya muziki azingatie masomo aweze kupata elimu itakayomsaidia mbele ya safari katika maisha.
AFANYA MUZIKI KWA SIRI
Nyota huyo aliendelea kusema kuwa akiwa sekondari,  aliendelea kuimba muziki lakini kwa siri kubwa ili mama yake asijue.
Mwaka 2004, anasema alianza kuandika nyimbo zake mwenyewe kwa kuwa akili bado ilimwambia mafanikio yake yatapatikana huko.
AFANYA VIBARUA APATE PESA
Mwaka 2006, Diamond alimaliza elimu ya sekondari na kuanza kuimarisha ndoto yake ya kuwa mwanamuziki.
Alikuwa hana kazi ya kufanya nyumbani hivyo alianza kutafuta vibarua mbalimbali vya kumuwezesha kupata riziki ya siku. Miongoni mwa kazi hizo ni kuuza mitumba, kuweka mafuta kwenye magari (vituo vya mafuta), kupiga picha, kupigisha simu na kazi za kwenye viwanda mbalimbali.
Je, unajua nini kiliendelea? Usikose Jumanne ijayo.

DIAMOND AKAMILISHA TAKEU KWA MADEMU...IDADI KAMILI YA ALIOWALA URODA HII HAPA !


Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ amekamilisha ‘TAKEU’ kwa mademu baada ya kufanikiwa kutembea na mademu wanaosifika kwa uzuri kutoka Tanzania, Kenya na Uganda.
Mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’.
Historia inaonesha dogo huyo kutoka Tandale aliwahi kufanya kazi na msanii mrembo kutoka nchini Kenya, Avril na ikadaiwa licha ya kukutana kikazi jamaa alimsaliti mpenzi wake wa enzi hizo, Penniel Mwingilwa.
Beautiful Onyinye, Wema Sepetu.
Aidha, Diamond amekuwa mpenzi wa Beautiful Onyinye, Wema Sepetu kwa muda mrefu kabla ya hivi karibuni wawili hao kuamua kupeana likizo.
Mdada anayetisha kwa uzuri na mkwanja nchini Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari’.
Katika kukamilisha TAKEU ambayo ni staili ya muziki ya Msanii Nice Lucas ‘Mr Nice’ inayogusa nchi hizo za Afrika Mashariki, Diamond juzikati alimnasa mdada anayetisha kwa uzuri na mkwanja nchini Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari’ na kufanya naye project ambapo inadaiwa wawili hao walivuka mipaka na kupeana penzi.

DIAMOND, ZARI GUMZO AIRPORT


Musa Mateja na Imelda Mtema
BAADA ya kula bata za kutosha Bongo, wakati wakisindikizana kimahaba, staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady, wamezua gumzo kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar, Ijumaa lina mchapo kamili.
Mrembo mkali kutoka Uganda, Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady (mwenye gauni jekundu) akishuka kutoka gari la ‘Diamond Platnumz’.
HABARI KAMILI
Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu lilijiri mishale ya mchana, Jumanne iliyopita katika maegesho ya airport (uwanja wa ndege) ambapo Diamond alikuwa akimsindikiza Zari aliyekuwa akitimua Bongo baada ya kufanya yao kwa siku kadhaa.
KABLA YA TUKIO
Awali kabla ya tukio hilo, gazeti hili lilipokea ‘ubuyu’ kutoka kwa chanzo chake cha kuaminika kwamba, wawili hao walikuwa wakijiandaa katika hoteli waliyokuwa kwa siku kadhaa iliyopo kwenye Ufukwe wa Bahari ya Hindi, tayari kuelekea uwanja wa ndege.
Zari au The Boss Lady akimwelekeza kitu mpambe wa 'Diomond'.
“Ijumaa acheni kulaza damu, kwa taarifa yenu Diamond ndiyo anajiandaa kumpeleka Zari airport wahini pale mpate tukio kamili ili kumaliza ubishi kuwa kweli walikuwa wote Bongo,” kilisema chanzo hicho kikiomba hifadhi ya jina gazetini.
IJUMAA MZIGONI
Baada ya kunyetishiwa ishu hiyo, wanahabari wetu walitia gia kwenye ‘motokaa’ ambapo dakika kadhaa baadaye walikuwa wametega satelaiti zao uwanjani hapo tayari kwa kunasa tukio.
Gari jeusi aina ya BMW X6 ya mkali 'Diamond' ikiendeshwa na mpambe wake aliyejulikana kwa jina la Q-Boy huku mwenyewe (Diamond) siti ya nyuma.
BMW X6 LATOKEA
Wakati wanahabari wetu wakiwa wanakaribia kukata tamaa, ghafla lilitokea gari jeusi aina ya BMW X6 ambalo tofauti na magari mengine, badala ya namba za usajili, lenyewe lilikuwa na maandishi yaliyosomeka kwa herufi kubwa ‘PLATNUMZ’ kisha likapaki kwenye eneo la maegesho uwanjani hapo.
Gari hilo lilikuwa likiendeshwa na kijana mmoja wa Diamond aliyejulikana kwa jina la Q-Boy na pembeni mwake kwenye siti ya abiria alikuwepo mpambe mwingine wa msanii huyo ambaye jina halikupatikana.
DIAMOND AJIFUNGIA
Wakiwa siti ya nyuma, wakati Zari anashuka, Diamond alijifungia kwenye gari ili kuwakwepa mapaparazi baada ya kuwashtukia kuwa walikuwa wakimsubiri.
Zari au The Boss Lady akisindikizwa na mpambe wa 'Diamond'.
WAZUA GUMZO
Wawili hao walizua gumzo uwanjani hapo ambapo baadhi ya watu wakiwemo Wazungu walikuwa wakiwashangaa huku Wabongo wakitamani Diamond atoke kwenye gari amtambulishe Zari kama ndiye mrithi wa Wema au la!
“Huyu Diamond naye balaa. Kampata wapi mtoto mrembo kiasi hiki? Hakyanani na mimi bora niwe msanii nitafaidi. Mtoto kaumbika hasa,” alisikika mmoja wa madereva teksi huku wenzake wakimkatisha tamaa kuwa hawezi kuwa msanii. Zari alishuka na yule mpambe wa Diamond na kuambatana hadi sehemu ya kukaguliwa ili akapande ndege.
Zari, 'The Boss Lady' akilonga jambo na paparazi wa gazeti la Ijumaa.
IJUMAA LAMBANA ZARI
Kabla ya kufikia sehemu hiyo, wanahabari wetu walibahatika kumfotoa picha za kutosha Zari kisha kumfuata na kumuuliza alikuwa na ishu gani na Diamond ambaye alikuwa naye hotelini Bongo kwa takriban siku tano.
Hata hivyo, Zari alishindwa kujibu na kuishia kusema kuwa hana maoni.“No comment,” alisema Zari na hata alipoombwa kufafanuzi kidogo aligoma.
DIAMOND AFUNGUKA
Baada ya tukio hilo, wanahabari wetu walimtafuta Diamond kwa njia ya simu ili azungumzie kwa kina juu ya uwepo wa Zari Bongo na tuhuma za kujihusisha naye kwenye mapenzi ambapo Diamond alifunguka:
Mbongo Fleva 'Diamond' wakati akitanua na Zari, 'The Boss Lady'.
“Niliwaona airport mkimpiga picha na gari langu na mkaongea naye.
“Kweli ninyi ni noma sana, lakini nadhani mliandika hivi karibuni kuwa mimi nimeachwa na Wema (Sepetu).
“Ukweli hakuna mwanaume anayeweza kujitoa kwa demu wake hasa kumpatia zawadi ya gari kama niliyotoa kwenye bethidei ya Wema halafu baadaye usikie kuna mwanaume mwingine katoa zaidi na ukaendelea kufurahia.
ZARI NI RAFIKI TU JAMANI!
“Sitaki kuongea mengi ila Zari naomba atambulike kama rafiki yangu tu jamani.”
YATOKANAYO
Hivi karibuni Diamond alimwagana na Wema ambapo siku chache baadaye habari zilivuja kwamba Zari ambaye ni msanii wa kike tajiri Afrika Mashariki ndiye mwenye uwezo wa kuziba pengo hilo mara tu baada kuonekana na jamaa huyo.
Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top