Habari Kali
Loading...

MASTAA BONGO MUVI NJAA TUPU!mas


Waandishi wetu
Imevuja! Uchunguzi uliofanywa na Ijumaa Wikienda umebaini kwamba mastaa wengi wa sinema za Kibongo wapo katika hali ngumu kiuchumi kutokana na soko la filamu kudorora huku wizi wa kazi zao na kusitishwa mikataba yao na makampuni makubwa ya usambazaji vikichangia.
Uchunguzi huo umebaini kwamba moja ya makampuni yaliyositisha mikataba ya wasanii ni Steps Entertainment ambao wamesababisha mastaa kibao kushindwa kutengeneza muvi kwa kuwa awali walikuwa wakipewa bajeti na Steps kisha kuwauzia kwa bei ya mapatano.
Ilibainika kwamba baada ya Steps kuachana na utaratibu huo na kudai kuwa wanachukua muvi zilizoandaliwa na makampuni binafsi za mastaa wachache kama Jacob Steven ‘JB’, Athuman Amri ‘Mzee Majuto’, Vincent Kigosi ‘Ray’ na wengine wenye makampuni binafsi.
Mmoja wa mastaa wakubwa wa filamu, Musa Issa ‘Cloud 112’ alikiri kuwepo kwa hali hiyo huku akifafanua kuwa Steps kuna wakati inakuwa kwenye kipindi kigumu.

MASTAA WA KIKE BONGO MOVIES MTAIGIZA MAISHA YENU HADI LINI?

Mastaa wa Bongo Movies. Bila shaka mko poa na mnaendelea na harakati zenu za kila siku, najua mna mishemishe nyingi kweli japo najua nyingi ni za starehe zaidi.Binafsi mimi niko poa naendelea na majukumu yangu ya kila siku ikiwemo hili la kuwaandikia barua. Madhumuni ya barua hii ni kama inavyojieleza hapo juu katika kichwa chake cha habari.
Ndugu zangu, nimekuwa nikifuatilia aina ya maisha mnayoishi kwa muda mrefu nimegundua wengi wenu mnaishi maisha ya kuigiza kama vile mnavyofanya kwenye filamu zenu. Hamtegemei kazi zenu kuendesha maisha bali mnatumia ‘njia’ mbadala ili kulinda heshima ya umaarufu wenu, siyo sawa.
Mnataka kuonekana mnakula katika mahoteli ya gharama, nyumba za gharama, kubadili mavazi kila siku, kuendesha magari ya kifahari na kila aina ya starehe mjini ili muweze kwenda sawa na wenye nazo.Ufahari mnaouonesha haufanani kabisa na pato mnaloingiza kwenye filamu (mifano ipo mingi tu).
Natambua kabisa bei ya sinema moja mnavyoiuza kwa wahindi au kwingineko, haitoshi kabisa kufanya vurugu ambazo mnazifanya kila siku wakati wengi wenu hata hamzalishi hata muvi tatu kwa mwaka.Dada zangu nataka tu niwakumbushe kwamba maisha si starehe tu, maisha yana maana kubwa kama mtajiheshimu na kutengeneza mazingira mazuri ya kutegemea kipato cha sanaa yenu, kuiboresha kwa kuwekeza nguvu na akili nyingi.

Sitaki kuwataja kwa majina kwa leo lakini naamini mnajijua. Kwa nini msifanye kazi kama baadhi ya mastaa wa kiume ambao tunawaona wanaingiza fedha na kuendesha maisha yao kupitia filamu wanazozizalisha? Kwa nini msiige mifano kutoka kwa dada zetu wa Nigeria ambao wanategemea sanaa kutengeneza mamilioni?
Badala msimame katika mfumo mzuri wa kuzalisha sinema kwa nguvu na akili zenu zote, nyinyi mnatumia njia ya mkato kujiingizia fedha. Madhara yake ndiyo mnajikuta mkiingia katika mtego wa kujiuza kama ilivyotokea kwa Jack Pentezel ‘Jack wa Chuz’, Aunty Lulu na Baby Madaha.
Ni rahisi mtu kuwarubuni kwa fedha, kuwanunulia magari ya kifahari na nyinyi mkaridhika na kuona mmeyapatia maisha. Kesho na kesho kutwa ndiyo haohao wanaokuja kuwanyang’anya baada ya kuwatumia vya kutosha sababu wanakuwa hawajawakabidhi kadi.
Ni aibu hata kwa mashabiki wenu ambao wanawafuatilia kupitia filamu. Wanavyoona mnaigiza maisha katika mitandao ya kijamii wanapata hamasa kwamba sanaa inawalipa kumbe kiuhalisia haiwalipi.Jamani badilikeni kwa kujituma katika kuigiza ili heshima ya majina yenu itokane na sanaa.
Naamini inawezekana kwani vipaji mnavyo na hakuna ubishi mnaweza kuibadilisha tasnia kama wenyewe mtaamua kufanya hivyo. Kwa leo acha niishie hapo, badilikeni!

Wasalaam
Erick Evarist

ESHE AWANANGA MASTAA BONGO MOVIE

Stori: Hamida Hassan
Staa wa filamu za Kibongo,  Eshe Buheti ameibuka na kuwananga mastaa wa kike waliobaki kwenye Kundi la Bongo Movie Unity kuwa hawajielewi na kazi yao ni majungu tu.Akistorisha na Risasi Jumamosi, Eshe alisema kuwa imefikia hatua baadhi ya wasanii hao hawasalimiani wanapokutana misibani kisa ni yeye kujitoa kwenye kundi, kituambacho haoni kama kina tija.
Staa wa filamu za Kibongo,  Eshe Buheti.
“Nawashangaa wasichana wenzangu naona hawajielewi tu ni kama vipofu kwani kwa ilipofikia mwisho tutapigana kwa sababu hata tukikutana misibani wananuna hiki ni kichekesho, mbona wakina Monalisa hawana kundi akina Riyama na wanafanya kazi kama kawaida? Badilikeni”, alisema Eshe pasipo kuwataja majina akidai wanajijua.

PIGO BONGO MUVI: MZEE MANENTO AFARIKI DUNIA

Mzee Manento enzi za uhai wake.
MSANII wa filamu za Kibongo, Mzee Manento amefariki dunia jana jioni akiwa jijini Dar es Salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Mzee Manento alikuwa akisumbuliwa na maradhi ya moyo na mpaka mauti yanamfika alikuwa amelazwa katika Hospitali ya TMJ iliyopo Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Mzee Manento atakumbukwa katika filamu alizocheza kama 'Hero of the Church', 'Dar to Lagos', 'Fake Pastor' na nyinginezo. Ndugu, jamaa na marafiki kwa sasa wamekutana nyumbani kwa marehemu huko Kigogo, Dar kujadiliana kuhusu taratibu za mazishi.
Mwenyezi Mungu ailaze Roho ya Marehemu mahali pema peponi. AMEEN!

MZEE CHILLO AGOMA KUZUNGUMZIA MAKUBALIANO YA UKAWA

Stori: Gabriel Ng’osha
MKONGWE katika filamu za Bongo, Ahmed Ollutu ‘Mzee Chillo’ amefunguka kuwa yeye si mwanasiasa hivyo hawezi kuzungumza chochote juu ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). Akijibu swali la mwandishi wetu baada ya kuulizwa anazungumziaje kitendo cha Ukawa kusaini makubaliano ya kusimamisha
Mkongwe katika filamu za Bongo, Ahmed Ollutu ‘Mzee Chillo’.
mgombea mmoja mmoja kuanzia ngazi ya serikali za mitaa mpaka uchaguzi wa urais utakaofanyika mwakani alisema: “Mimi siyo mwanasiasa, huwa nafuatilia kujua wamezungumza nini, tena siyo sana kisha naachana nao, niulize kuhusu sanaa, hata kama niko usingizini nitakujibu kwa sababu ndiyo kazi yangu,’’ alisema Mzee Chillo.

DAVINA: BONGO MOVIE HAIJANIPA MUME

Stori: Gladness Mallya na Hamida Hassan
MSANII wa filamu Bongo, Halima Yahya ‘Davina’ amesema wanaomsimanga kuwa amepata mume kwa sababu yao hawana hoja kwa sababu Bongo Movie Unity haina ubavu huo.
Msanii wa filamu Bongo, Halima Yahya ‘Davina’.
“Mimi sijatafutiwa mume na Bongo Movie, alinitafuta mwenyewe baada ya kuniona kwenye muvi yangu ya Tone la Damu akiwa Italia, sasa nashangaa na ninaumia ninaposikia eti Bongo Movie walinitafutia.
“Ukweli naombeni mniache kwa sababu hakuna aliyehusika kwa kitu chochote kunikutanisha na mume wangu, hivyo acheni kunisengenya na mimi siringi kwa chochote kama ni kutoka huko kwenye kundi ni maamuzi yangu maana sikuwa naona faida yoyote,” alisema Davina.

‘UKAWA’ YAZALIWA BONGO MOVIE

Stori: Gladness Mallya na Gabriel Ng’osha
WASANII wa filamu ambao hivi karibuni waliripotiwa kujitoa katika kundi la Bongo Movie Unity wamedaiwa kuunda la kwao linalojulikana kama Ukawa ambalo litakuwa chini ya uongozi wa Mwenyekiti aliyetimuliwa, Steven Mengere maarufu kama Steve Nyerere.
Baadhi ya Wasanii wa bongo Movies waliokuwa pamoja katika uongozi kabla ya mzozano.
Baadhi ya wasanii wanaotajwa kuunda kundi hilo kwa mujibu wa chanzo chetu makini ni pamoja na Devotha Mbaga, Salama Salmin ‘Sandra’, Halima Yahya ‘Davina’ na wengineo.
“Yaani sasa hivi haya makundi mawili kuna vita kali sana, kila moja linataka lionekane kwamba lina nguvu kuliko lingine, hata jina la Bongo Movie Unity limebadilishwa sasa hivi linaitwa Bongo Movie Stars,”kilisema chanzo hicho.Aliyekuwa Katibu msaidizi wa Bongo Movies Unity, Devotha Mbaga.
Mussa Issa ‘Cloud’ alikiri kubadilishwa jina kwa Bongo Movie Unity na pia amesikia habari za kuwepo kwa kundi la Ukawa wakati Steve Nyerere alisisitiza kuwa bado ni mwanachama wa Bongo Movie Unity na kwamba mtu anayetaka kuwagombanisha wasanii anajulikana.

STEVE NYERERE AFUTWA UANACHAMA

Stori:  Deogratius Mongela
Mshtuko! Siku chache baada ya kujiengua kwenye nafasi ya uenyekiti katika Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ anadaiwa kufutwa uanachama wa klabu hiyo.
Aliyekuwa mwenyekiti katika Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Chanzo cha ndani ya klabu hiyo kimepenyeza madai kuwa, wameamua kumvua uanachama Steve kwani wanaona ni ‘kirusi’ ndani ya klabu kutokana na mwenendo wake.
“Steve amekuwa akiwashawishi baadhi ya memba wajiunge na upande wake, tofauti na umoja wa Bongo Movie Unity, viongozi wameamua kumfuta kabisa uanachama,” kilisema chanzo na kuongeza:
“Amewatangazia wenzake vibaya juzikati alivyokwenda Dodoma kwenye sherehe za kukabidhiwa kwa Rasimu ya Katiba Iliyopendekezwa kwa kuwaambia viongozi wa serikali kwamba wasanii ambao hawakwenda mjini humo ni Ukawa wakati si kweli.”
Katibu wa Bongo Movie Unity,William Mtitu akiwa ndani ya Ofisi za Global.
Baada ya chanzo chetu kujiridhisha na data hizo za ndani, mwanahabari wetu alimtafuta Steve Nyerere ili kujua anazungumziaje juu ya ishu hiyo ya kuenguliwa klabuni na mtazamo kuhusu suala hilo, alipopatikana alikuwa na haya ya kusema:
“Mimi ni mwanachana wa Bongo Muvi kama nimefutwa sijui lakini ni mwanachama. Kuhusu kuwasemea nilipokuwa Dodoma, ningewasemea mimi kama nani? Sina cheo cha kuwasemea wenzangu.
Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na tafrani kubwa Bongo Muvi huku madai mengi yakielekezwa kwa Steve.

DK. CHENI: RUSHWA YA NGONO WANAITAKA WENYEWE!

Stori: Gladness Mallya
KASHFA! Staa wa filamu za Kibongo, Muhsein Awadhi ‘Dk. Cheni’ amekanusha tabia ya wasanii wakubwa kuwaomba rushwa ya ngono wasanii chipukizi na kudai wanaziendekeza wao wenyewe.
Staa wa filamu za Kibongo, Muhsein Awadhi ‘Dk. Cheni’.
Akipiga stori na paparazi wetu, Dk. Cheni alisema yeye hajawahi kumuomba msanii rushwa ya ngono, isipokuwa anaamini walio wengi huanzisha mahusiano yaliyo rasmi kwa makubaliano yao kutokana na hisia zinavyowasukuma.
“Sizani kama ni rushwa ya ngono, naamini wengi wanakubaliana, sehemu ya watu wengi mnapokutana inatokea watu kupendana na kuwa wapenzi hilo nakubali sababu ni jambo la kawaida hata wasanii kwa wasanii kupendana, sidhani kama mtu anaweza kulazimishwa kufanya mapenzi ili acheze filamu, mpaka watu kufanya tendo hilo wameshakubaliana,” alisema Dk. Cheni.

LULU: BONGO MOVIES ISHABUMA

Stori: Imelda Mtema
STAA wa filamu mwenye makeke mengi, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema kwa mtazamo wake anaona Bongo Movies imebuma hivyo ameamua kukomaa na shule ili awe na kitu kingine tofauti na sanaa.
Staa wa filamu mwenye makeke mengi, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Lulu alisema kuwa kwa sasa yuko Chuo cha Uhazili Magogoni, Posta jijini Dar akichukua ‘course’ ya Utawala wa Umma (Public Administration) kwa ajili ya kupata ujuzi mwingine kichwani.
“Mwe-nzangu naona Bongo Movies kunaelekea kubaya, bora hata nikomae na shule angalau hata niwe na kitu kingine kichwani nipate mbadala wa sanaa,” alisema Lulu.

MIKE ADAIWA KUWA MLINZI WA STEVE NYERERE

Na Hamida Hassan
STAA wa filamu za Bongo, Mike Sangu amedaiwa kuajiriwa na Steve Nyerere kuwa mlinzi wake kutokana na kutembea naye kila kona.
Staa wa Filamu za Bongo, Mike Sangu
Chanzo cha habari hii kilidai kuwa, baada ya Steve kuachia madaraka Bongo Movie Unity, Mike naye alijiondoa kimyakimya na kuhamia kwa Steve na kuwa mlinzi wake kila anakokwenda.
“Unajua hadi aibu! Steve hata akisogea kwenda kuongea na simu Mike anamfuata na kukaa nyuma yake. Nadhani jamaa atakuwa kamuajiri,” alisema mtu mmoja ambaye hakupenda jina lake litoke gazetini.
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bongo Movie Unity, Steve Nyerere(aliyenyoosha mkono)
Mike alipoulizwa kuhusu madai hayo alikiri kuwa sambamba na Steve kwa sababu wametoka mbali lakini alikanusha kuwa mlinzi wake.

MAMA KANUMBA, LULU NDANI YA FILAMU MPYA IITWAYO 'MAPENZI YA MUNGU'

Hivi karibu Msanii Mahiri na Nguli katika tasnia ya filamu nchini Elizabeth Michael almaarufu kama LULU ataibuka na filamu yake Mpya na yenye kusisimua iitwayo 'MAPENZI YA MUNGU' ambapo moja kati ya washiriki katika filamu hiyo ni Bi Flora Mtegoha ambae ni Mama Mzazi wa aliyekuwa Msanii Nguli wa Kiume Hapa Bongo Marehemu Steven Kanumba.
Filamu ya 'Mapenzi ya Mungu' ni moja ya filamu ambayo Lulu ameonyesha uwezo wa hali ya na kuthibitisha kuwa ni mmoja kati ya wasanii wa kike hapa Tanzania ambae ana kipaji cha hali ya juu katika kuuvaa uhusika ambapo ana uwezo wa kubadilika badilika kutokana na muongozo anaopewa.
Filamu ya 'Mapenzi ya Mungu' itakuwa Sokoni hivi Karibu Kwa Wauzaji wa Filamu kote Nchini.
Filamu hii itasambazwa na Kampuni mahiri ya Proin Promotions Ltd.

KAJALA YAMKUTA BAADA YA KUWEKA PICHA SIMU AMBAYO BADO HAIJATOKA SOKONI AKIDAI ANAYO, WATU WAMCHANA HIVI



Kajla1b- bongoclan.co.tz
Kupitia mtandao maarufu wa picha wa kijamii, mwanadada Kajala amejikuta kwenye wakati mgumu baada ya kuweka picha ya simu aina ya samsung galaxy note 4 kwenye account yake kuwa anamiliki simu hiyo ilihali simu yenyewe ikiwa bado hata haijaanzwa kuuzwa sehemu yoyote duniani. Kupitia picha hiyo kajala aliambulia maneno kadhaa ya kashfa toka kwa watu mbalimbali wengi wao wakimtaka aache maisha ya kuigiza.
IMG_20141009_104812
Baadhi ya maoni hayo ni:-
“Hahahaha watu ndo wanatoa pre order october 16 ndo ina launched we umeitoa wap wakat bado haijaanzwa kuuzwa!dah!kwel sasa naanza kumin maisha yako ni ya kuigiza nakufata mkumbo mumy…pole”
“Duh … Simu aijatoka hiyo Pre Order imeanza USA & UK tarehe 19/09 lkn retail stores wanaanza kuuza tarehe 17/10 , hiyo pre order kwa watu ambao awataki kumiss ikitoka wanalipia kabisa ikitoka unaenda kuchukua , sasa hiyo umenunua wapi mwenzetu…”
“KAJALA ACHA UONGO HII CM LABDA MCHINA ORIGINAL HAIJATOKA MPKA KWA ORDER LOO MWANAMKE MZIMA MPKA LEO UNARINGISHIA CM PAULA NAE AFANYE NINI”
Wewe unaonaje kuhusu jambo hili la mastaa nchini kuishi maisha ya kuigiza kwa ajili ya kuonekana wapo juu kwa mashabiki wao?
   

MILIONI 30 ZA JOHARI ZIMEPOTEA BAADA YA KUZUILIWA KUTOKA KWA FILAMU YA SISTER MARRY




Muigizaji wa filamu Blandina Chagula aka Johari amesema pamoja na kusikitishwa kutokana na bodi ya filamu nchini kuizua filamu ya ‘Sister Marry’ isitoke, amekula hasara kubwa.

Johari amesema  kuwa maandalizi ya filamu hiyo yalighalimu shilingi milioni 30.
 
“Unajua inauma sana, tumeshindwa kutetea filamu ya ‘Sister Marry’ kutokana na madai eti tumedhalilisha dini. Ina maana hawataki tuzungumzie maisha halisi kwenye filamu zetu? 
 
"Mimi binafsi imeniumiza sana. Ile filamu imegharimu zaidi ya milioni 30, hebu angalia, Halafu inafungiwa ili isitoke kabisa!
 
"Kinachonisikitisha ni kwamba serikali yetu inashindwa kuangalia sisi tunavumbua baadhi ya maovu ya watu ambayo wanayafanya ili kuelimisha jamii.
 
"Kwahiyo imefungiwa na kukatazwa isitoke kabisa kwa sababu kuna mambo ya ukweli ambayo tumeyaonyesha.

"Tumefanya kila njia mpaka sasa hivi tumeshindwa, kwahiyo filamu ya Sister Marry haitatoka tena,” amesema Johari.
   

MBONGO MOVIE BUNGENI ANUSURIKA KIFO

Stori: Hamida Hassan
Mwakilishi wa wasanii katika Bunge Maalum la Katiba (BMK), Paul Mtenda juzikati alinusurika kifo baada ya gari lake kugongana uso kwa uso na lingine katika eneo la Dumila mkoani Morogoro wakati akirejea jijini Dar es Salaam kutoka Dodoma.
Mwakilishi wa wasanii katika Bunge Maalum la Katiba (BMK), Paul Mtenda.
“Namshukuru Mungu sikuumia kwa sababu nilikuwa nimefunga mkanda, lakini kile kilikuwa ni kifo kwangu,” alisema mwakilishi huyo, mmoja wa wajumbe waliopitisha Katiba Mpya ya nchi inayopendekezwa.
Muonekano wa gari hilo baada ya ajali.
Kutokana na kunusurika huko, Paul alisema alilazimika kufanya maombi maalum kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kumuepusha na kifo, licha ya gari lake kuharibika vibaya.

CLOUD AKANA KUMFITINI FRANK

Stori: Mayasa Mariwata na Chande Abdallah
MSANII mkongwe wa filamu Bongo Issa Musa ‘Cloud’ amekana tuhuma zinazosambazwa mtandaoni kuwa alimfitini muigizaji mwenzake, Mohammed Mwikongi ‘Frank’ ili kumzuia asisafiri kuelekea Uingereza miezi michache iliyopita.
Msanii mkongwe wa filamu Bongo Issa Musa ‘Cloud’.
“Mimi sikumfitini Frank, yule mtu alinifuata mwenyewe kwa makubaliano ya mdomo kuwa nikacheze filamu, sikuwa peke yangu, tuliongozana na kina Monalisa na Riyama, tatizo ni la huyo aliyenipeleka kule, nilifanya mambo kwa mazoea na ndiyo sababu anaamua kusambaza uongo dhidi yangu,” alisema mkongwe huyo wakati akizungumza na Global Tv.
Msanii mkongwe wa filamu Mohammed Mwikongi ‘Frank’.
Aliwasihi wasanii wenzake nchini kuacha kufanya kazi kwa mazoea bali wahakikishe wanaingia mikataba ya maandishi ili wawe na ushahidi wakati waliokubaliana nao kazi wanapoleta ujanjaujanja kama ilivyomtokea yeye katika safari hiyo ya Uingereza ambayo sasa inamletea uadui na Frank.

MASTAA WAJIENGUA BONGO MUVI


Stori: Hamida Hassan na Imelda Mtema
HALI bado tete! Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Klabu ya Bongo Movie Unity, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ kujiuzulu, upepo mbaya unaendelea kuitafuna klabu hiyo ambapo sasa wasanii wengine watano wamejiengua, Risasi Mchanganyiko linakupa mchapo kamili.
Msanii wa filamu Bongo, Halima Yahya ‘Davina’.
Kutokana na wasanii hao kujitoa, klabu hiyo inaonekana kupoteza muelekeo ambapo kwa sasa wanachama waliobaki kundini wanajipanga upya ili kuisimamisha upya.
Kwa mujibu wa chanzo makini, wasanii waliojiengua ni Halima Yahya ‘Davina’, Esha Buheti, Kajala Masanja, Flora Mvungi na  Salma Salmini ‘Sandra’ huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni kukithiri kwa vitendo vya ngono na ubaguzi wa kimaslahi.
Msanii wa filamu Bongo, Flora Mvungi akipozi.
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu kwamba, hivi karibuni kulitokea safari ya wasanii kwenda mkoani Tanga lakini baadhi ya viongozi wamedaiwa kujichagua kwa ‘kapo’ bila kujali kuwa wapo wanachama wengine ambao wanatakiwa kwenda huko.
Kikifafanua madai hayo, chanzo hicho kilikwenda mbele zaidi na kuzinadi kapo hizo kama ifuatavyo:
Cloud 112 (Issa Musa) alidaiwa kuongozana na Coletha Raymond, JB (Jacob Steven) na Shamsa Ford, Rose Ndauka na Single Mtambalike (Rich) na wengine.
Msanii wa filamu Bongo, Kajala Masanja.
Baada ya madai hayo kutua kwa mapaparazi wetu, walianza kwa kuwatafuta walengwa ambao wamedaiwa kubaguliwa na kuamua kujitoa klabuni hapo. Mambo yalikuwa hivi:
Davina:
“Mimi nimeamua kujitoa kwa sababu naona mambo mazuri wanachaguana mapatna tu sisi tunakumbukwa pasipo mazuri, kwenye pesa wanapeana wao wenyewe, mimi mpaka mume wangu alikuwa akiniuliza kwamba napata faida gani.”
Msanii wa filamu Bongo, Salma Salmini ‘Sandra’
Sandra:
“Sijapata faida yoyote Bongo Movie, watu wanapeana mapatna inapotokea suala la safari na pesa.”
Esha Buheti:
“Mimi nimeamua kujitoa kwani watu wamekuwa na ubaguzi, sisi tunaitwa unapotokea msiba tu, nitafanya kazi zangu mdogomdogo, nitatoka tu.”
Msanii wa filamu Bongo, Esha Buheti.
Kajala:
“Nimejitoa kwa sababu kule nilikuwa nikimfuata Steve Nyerere, sasa ameshatoka nafuata nini tena?”  
Jitihada za kuwapata wasanii wanaotajwa kuwa ni wabaguzi ziligonga mwamba kwa baadhi ya wasanii lakini alipopatikana Cloud 112, alikanusha taarifa hizo.
“Hakuna kitu kama hicho, sisi tunasafiri kulingana na matakwa ya waandaaji wa safari, waandaaji ndiyo wanaosema wanamtaka nani katika shughuli yao, wanaosema hivyo wamekosa la kuongea,” alisema Cloud 112.

BUSU LA BATULI, CHILO UTATA!


Stori: Gladness Mallya
MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’ amezua utata wa aina yake kufuatia kunaswa akimpiga busu matata mkongwe, Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’.
Mwigizaji wa sinema za Kibongo, Yobnesh Yusuph ‘Batuli’
Baada ya picha inayowaonyesha wawili hao wakiwa ‘very close’ wakifanya tendo hilo kunaswa na paparazi wetu, paparazi wetu alimtafuta Batuli na kumuuliza kulikoni?
Mkongwe katika tasnia ya filamu Bongo, Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo’
“Aaah wewe acha mambo yako, busu la kawaida hilo bwana hakuna cha ziada, tulikuwa katika sherehe flani hivi Dodoma ndipo nikajikuta tu nimempiga busu,” alisema Batuli.

MTITU AFUNGUKIA BIFU LAKE NA STEVE

Stori: Gladness Mallya
BAADA ya tetesi kuzagaa kwamba aliyekuwa Katibu wa Bongo Movie Unity, William Mtitu kwamba ana bifu kali na aliyekuwa mwenyekiti wa kundi hilo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ mwenyewe amefunguka kwamba hawezi kufanya kitu kama hicho.
Aliyekuwa Katibu wa Bongo Movie Unity, William Mtitu.
Akistorisha na paparazi wetu, Mtitu amesema anashangazwa na taarifa hizo licha ya kwamba hawajawahi kuzungumza na Steve tangu alipoachia ngazi ya ukatibu.
“Sijawahi kutishia kuua mtu kama watu wanavyosema, Steve ni mdogo wangu hivyo kama atakuwa na bifu na mimi ni yeye na sitajali kwani wangekuwa ni kina Ray au wasanii wengine wakubwa wamenichunia ningewaza lakini huyo haniumizi kichwa,” alisema Mtitu.
Aliyekuwa mwenyekiti wa kundi hilo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
Maddi yaliyopo mtaani ni kwamba, wasanii hawa kwa sasa ni kama paka na panya na imefika hatua ya kutishiana kuuana.

Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top