Habari Kali
Loading...

Wema Sepetu 'Mimi SINA Kinyongwa na DIAMOND ila Yeye Ndio Anakinyongo na MIMI, Nilimwandikia Message Kumpa Pole ila Hakunijibu'

Akizungumza kwenye kipindi cha Ubaoni cha EFM leo, Wema alisema kuna siku alimtumia ujumbe wa simu Diamond kumpa pole kwa kumuuguza mama yake lakini alimchunia.

“Tumeshaachana kwanini tuwekeane grudges,?”alihoji Wema kwenye kipindi hicho. “Tulikuwa pamoja lakini tumeachana kwanini tuwekeane bif, kinyongo? Mimi leo na kesho nikutana na mtu kama Jumbe siwezi kumpita nikasema nisimsalimie! Nikutana na mtu kama Chaz Baba, Chaz Baba mara ya mwisho juzi kaja nyumbani kaja kaniona alikuwa kaniletea kambwa tuongea kishkaji! Kwahiyo kama ulikuwa na mtu halafu mkaachana hamtakiwi kuwekeana kinyongo,” alisisitiza.

Mimi siwezi kuwa na kinyongo na Diamond hata siku moja lakini imekuwa iko tofauti kwa sababu mwenzangu hayuko hivyo anataka ile no! No! sijui ni kwa nini lakini labda kila mmoja ana jinsi anavyofikiri.”

Sijawai kumpigia simu ila nilishawakumtext, nilisikia kwamba mama yake anaumwa baada ya kusikia mama yake anaumwa nilim-text kama pole kwa sababu sina kinyongo naYe nikampa pole lakini kama nilivyoowambia mwenzangu yupo tofauti, nilifanya kibinadamu yule mama mimi hajanikosea.

WEMA, WOLPER WALEWA CHAKARI!

Sifael Paul
Hatari! Masistaduu wawili kunako gemu la Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Jacqueline Wolper Massawe, wamejikuta wakipiga ulabu hadi kulewa chakari, kisa kikielezwa kwamba wana msongo wa mawazo, Risasi Jumamosi linafunguka.
Masistaduu wawili kunako gemu la Bongo Movies, Wema Isaac Sepetu na Jacqueline Wolper Massawe wakipiga mtungi usiku mnene.
ENEO LA TUKIO KINONDONI-MANYANYA
Tukio hilo lililoshuhudiwa na gazeti hili lilijiri hivi karibuni, usiku mnene kwenye pati ya kuzaliwa (birthday) ya meneja wa kampuni ya Wema ya Endless Fame almaarufu Petit Man iliyofanyika kwenye nyumba ya jamaa mmoja maeneo ya Kinondoni-Manyanya jijini Dar na kuhudhuriwa na mastaa kibao.
Katika pati hiyo ambayo mbali na mastaa ilihudhuriwa na watoto wa mjini, watu waligonga msosi wa kufa mtu kisha vikafuata vinywaji.
Tofauti na ‘maraia’ wengine, Wema na Wolper walikuwa wakigonga vinywaji vikali hadi wakawa tilalila na kuanza kufanya vituko, jambo ambalo liliwashangaza wengi.Kadiri muda ulivyokuwa unasonga ndivyo mastaa hao walivyozidi kucharuka tofauti na walipofika kwani walionekana wapole na wastaarabu kupita maelezo.
Baada ya ulabu kuwakolea walianza kupigana picha kwa simu kisha kukata mauno kabla ya Wolper kuzimika kufuatia kuzidiwa na ‘kinywaji’.Kwa upande wake Wema alimpiga vibao mwanaume shoga aliyetajwa kwa jina moja la Danny baada ya kutibuana kabla ya watu kuwaamulia.Ulipofika muda wa kuondoka mahali hapo, ilidaiwa kwamba Wolper ilibidi abebwe ili kupelekwa kwenye gari kwani alikuwa hajiwezi.
Wema Isaac Sepetu na Jacqueline Wolper wakifurahia jambo.
KISA MSONGO WA MAWAZO
Uchunguzi wa Risasi Jumamosi umebaini kwamba, mastaa hao wana msongo wa mawazo hivyo wanaona njia pekee ya kuwaondolea ‘stresi’ ni kunywa pombe.
WEMA
Habari za ndani zilieleza kwamba, tangu Wema ameachana na staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amekuwa mtu mwenye mawazo na njia pekee ambayo huitumia ni kujipooza kwa pombe kali.
“Ndiyo maana ana mpaka kaunta ya pombe kali nyumbani kwake,” alisema mmoja wa watu wake wa karibu (Team Wema).
ZARI ATAJWA
Ilisemekana kwamba mbali na mawazo ya Diamond ambaye amehamia kwenye nyumba ambayo Wema alikuwa na mchango mkubwa wakati wa ujenzi, pia suala la jamaa huyo kutanua na mpenzi wake wa sasa, Zarinah Hassan ‘The Boss Lady’ limekuwa likimpa wakati mgumu mwanadada huyo.
Staa katika tasnia ya filamu, Bongo Wema Isaac Sepetu.
SUALA LA UGUMBA
Habari zilieleza kuwa, jambo lingine linalompa Wema msongo wa mawazo ni suala la kukosa mtoto kila anapomtafuta akiamini kuwa watu wanajua yeye ni mgumba.Pia ilielezwa kwamba kuna suala la kuishiwa na kuogopa kufilisika kwani kwa sasa filamu hazilipi na bado anataka kuendelea kuwa na heshima ya kuitwa Madam hivyo njia pekee anayoona inafaa kutuliza mawazo ni kunywa pombe.
WOLPER
Kwa upande wake Wolper uchunguzi ulionesha kwamba, kwanza anapenda fedha hivyo kukosa tenda za kuigiza na kuanguka kwa soko la filamu za Kibongo kumemsababishia msongo wa mawazo kama ilivyo kwa Wema kwani naye anataka kuishi maisha ya kistaa ambayo hayawezekani bila kuwa na mshiko.
WOLPER KALOGWA?
Akizungumzia hali hiyo, Wolper alikiri kuwa na mawazo mengi huku akihisi kuwa huenda amelogwa.
USHAURI WA KISAIKOLOJIA
Staa katika tasnia ya filamu, Bongo Jackline Wolper.
Kwa mujibu wa mtaalam wa saikolojia aliyezungumza na gazeti hili juu ya mastaa aliwashauri kama ifuatavyo;
Mtaalam huyo alishauri mastaa hao kuachana na pombe na kama wana mawazo ya kuumiza, wanatakiwa kujilazimisha kutabasamu mara kwa mara na kusahau jambo linalowaletea mawazo mabaya.
Alisema kuwa, kutabasamu kutawasaidia kuchangamsha akili, ingawa inaweza kuchukua muda kurudi katika hali ya kawaida lakini inasaidia kuamsha hisia za furaha zilizokuwa zimeshambuliwa na mawazo mabaya na kuamini katika ushindi.
WASISAHAU NYUMBA ZA IBADA
Pia aliwashauri kusahau mambo yaliyopita na kujikita katika kufanya kazi kwa bidii hata kama matunda hawayaoni sasa, yatakuja baadaye.Mbali na hivyo wajitahidi kujichanganya katika makundi ya watu sahihi na kujumuika kwenye nyumba za ibada, msikitini (kwa muislam) na kanisani (kwa mkristo).

Kauli ya Wema Sepetu Yawaliza Wengi. Aweka wazi kuwa hawezi kupata mtoto

.


Kupitia ukurasa wake wa instagram,  mwanadada wema Sepetu ameamua kuvunja ukimya kwa kuamua kuweka wazi kuwa hana uwezo wa kushika ujauzito... hiki ndicho alichosema!
 
"Ningekuwa na uwezo wa kuzaa ningekuwa nimezaa muda mrefu sana... But sina... Na siwezi kumkufuru mwenyezi mungu.... Au mngependa niwe nawaambia jinsi ninavyo hangaika usiku na mchana kupata mtoto wangu mwenyewe... Is dat wat u want...? kila ntakachofanya kwa ajili ya tumbo langu basi nitangaze... Au mnadhani siumii mnavyosema kuhusu maswala ya mtoto...
 
"Kumbukeni na mimi pia ni binaadam... Nina moyo kama nyie... Au mnadhani napenda kuona wenzangu wana watoto au wana ujauzito alafu mimi sina hata wa kusingiziwa... Mnaona nafurahia sio.... Hivi mna nini jamani..
 
"Yaani mtu unaweza weka post kwa nia nzuri then people jus come from nowea wanaanza kukuandikia maneno ya kukuumiza kabisa nafsi hadi mtu unakaa unajiuliza umemkosea nini mwenyezi Mungu...
 
"Kwani kuna niliemkosea yoyote mpaka muanze tu kunikashif na kunitolea maneno mazito namna hio... Kisa mtoto... Mnadhani naipenda hii hali...
 
"Hata mimi natamani kuitwa mama na hakuna kinachoniuma kama hicho.... So mnadhani sijui kama umri unaenda na maisha yenyewe sikuhizi mafupi anytime we die... Mnafikiria nisingependa kuacha hata ka copy kangu siku ndo Mungu anasema ananichukua...
 
"Hata mimi natamani ningekuwa napiga picha niko na mwanangu... I want dat with all my life but I cant.... Sitokaa nimkufuru Mungu wangu hata siku moja maana sijui ni kitu gani kaniandikia... But just dont rub it in... It hurts... And im jus a human being like each and every one of u....

 src-Mpekuzi blog

WEMA AKATAA UNAFIKI, AMPONGEZA CHIBU


Imelda Mtema
Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Sepetu amefunguka kwa mara ya kwanza na kusema kuwa hata yeye anampa pongezi mpenzi wake wa zamani, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kwa jitihada alizozifanya mpaka kufikia hatua ya kumaliza nyumba yake iliyopo Madale jijini Dar.
Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Sepetu.
Akizungumza na gazeti hili juzi, Wema alisema kuwa hata kama hawako pamoja lakini kama kuna kitu cha kumsifia kwa jambo zuri alilofanya hana sababu ya kukaa kimya na akinyamaza atakuwa mnafiki.
“Nikikaa kimya bila ya kumpongeza Chibu nitakuwa mnafiki, amefanya jambo zuri la kuigwa hivyo binafsi nampongeza kwa hapo alipofikia,” alisema Wema ambaye katika hatua za mwanzo za ujenzi huo alishiriki.

"Mimba My Foot"... Mashabiki wa Zari (Mpenzi wa Diamond ) Wamvaa Wema Sepetu baada ya kukejeli Mimba Yake


Wema Sepetu anahisi ujauzito wa Zari The Boss Lady ni geresha tu, hakuna lolote!

Hii ni kwa mujibu wa picha inayoonekana kuwa iliwekwa kwenye ukurasa wa Instagram wa Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 na ex wa Diamond Platnumz.
 
Picha hiyo haipo tena lakini Zari alifanikiwa kuipata na kuiweka kwenye ukurasa wake  wa  pili (zarithebosslady_) kuelezea alivyosikitishwa na kauli ya Wema kwenye picha yake (Zari) isemayo ‘mimba my foot’. 
 
Kwa mujibu wa urbandictionary.com msemo ‘my foot’ humaanisha: An exclamation that means that one believes the previous speaker’s statement to be untrue
 
Mrembo huyo wa Uganda anayetarajia kumzalia Diamond mtoto wake wa kwanza, aliipost picha hiyo na kuifuta tena baadaye na kuandika: 

"Astagafululah! May God Protect Zarimond and chibu junior #zaritlale #chibujunior #zarihassan #chibudangote"

WEMA, AUNT KICHEKO KABURINI KWA NGWEA

Stori: Musa Mateja
INAWEZEKANA ilikuwa utani? Au ‘waliamka’ nazo?! Kweli binadamu anaweza kuvunjika mbavu (kicheko) juu ya kaburi la mpendwa wake? Mh!
Mastaa wa Bongo, Wema Sepetu na shostito wake, Aunt Ezekiel wakiangusha kicheko katika kaburi la marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’.
Lakini imetokea! Wakati dunia ikisherehekea ujio wa mwaka mpya wa 2015, mastaa wa Bongo, Wema Sepetu na shostito wake, Aunt Ezekiel walionesha jambo tofauti kufuatia kutinga kwenye kaburi la aliyekuwa nyota wa Bongo Fleva, marehemu Albert Mangweha ‘Ngwea’ na kutumia muda mwingi kucheka na kutuma meseji kwa simu wakiwa juu ya kaburi hilo.
ENEO LA TUKIO
Tukio hilo lililonaswa zimazima na kamera za Risasi Jumatano, lilijiri Januari Mosi, mwaka huu kwenye kaburi la Ngwea lililopo katika Makaburi ya Kihonda mjini Morogoro.
ILIVYOKUWA
Aunt ndiye aliyeanza kutia timu kwenye makaburi hayo na kukaa. Baadhi ya ‘kruu’ ya Wema, akiwemo Petit Man nayo ilifika na kuungana na Aunt.Baada ya dakika tatu, Mama la Mama, Wema aliwasili akiwa ndani ya nguo isiyokuwa ya mtoko, akakaa upande wa pili wa kaburi. Yeye na Aunt walikaa kwa kupeana ubavu.
CHA AJABU SASA
Awali ilidaiwa kuwa, kruu hiyo ilipanga kuwa baada ya kufika kwenye kaburi hilo wangefanya dua fupi kwa ajili ya kumwombea marehemu apumzike kwa amani huko aliko.Lakini cha ajabu, kabla ya ibada hiyo, Wema, Aunt na wafuasi wao walikuwa wakipiga stori za hapa na pale na katika hali ya kushangaza zaidi, ilifika mahali wakaanza kucheka kile kicheko cha kuvunjika mbavu bila shuhuda wa tukio hili kujua nini hasa kilichokuwa kikiwachekesha!
...Wakizidi kucheka katika kaburi hilo.
Baadhi ya wapita njia waliokuwa wakikatiza karibu na makaburi hayo, nao walipigwa na butwaa kuwaona watu hao, walioamini ni ndugu wa marehemu, wakiangua vicheko kama hawana akili nzuri. kwa nukta kadhaa walisimama na kushangaa kabla ya kuendelea na ‘hamsini zao’.-
WEMA ATUMIA SIMU KUFICHA USO
Ni dhahiri kuwa, Wema alijishtukia kuwa kitendo cha kucheka juu ya kaburi hakikuwa na ujazo wa kiungwana hivyo haraka sana aliweka simu sehemu ya midomoni na kumfanya asionekane kwenye kamera kwamba alikuwa akicheka. Miwani ya jua aliyovaa pia ilimsaidia.
Wakati Wema akionesha ubinadamu huo, ‘mwenzangu na mimi’, Aunt yeye alijimalizia kiu yake ya kicheko mpaka pale alipoamua mwenyewe kuacha na si kwa kuogopa kamera wala malaika waliolizunguka kaburi lile (kama wapo) la mmoja wa marapa bora kabisa kuwahi kutokea Tanzania.
WEMA AJIELEZA KWA RISASI
Baada ya wote kuacha kucheka na kila mmoja kuchukua nafasi ya ubinadamu, paparazi wetu alimuuliza Wema ni kwa nini walionesha kuwa na furaha juu ya kaburi la staa huyo.Wema: “Tumepita hapa ili kumuombea ndugu na rafiki yetu Mangweha hivyo hatuna lengo lingine zaidi ya hilo.“Ishu ya kupiga stori na kucheka, tusingeweza kuacha kuongea eti kisa tupo kaburini, maana kila kitu lazima kijadiliwe hata kukaa hapa tumekaa kwa sababu tunafarijika kuona kaburi la mwenzetu.”
Albert Mangweha ‘Ngwea’ enzi za uhai wake.
KWA NINI WALIFANYA ZIARA KABURINI KWA NGWEA?
Awali, mastaa hao na wapambe wao walikuwa na shoo ya kuukaribisha Mwaka Mpya iliyofanyika Desemba 31, 2014 ndani ya Ukumbi wa  Matei Lounge mjini Dodoma.Wakiwa wanarudi Dar, walipiga kituo mjini Morogoro ambapo miongoni mwa mambo waliyokuwa nayo kwenye ratiba ni kulitembelea kaburi la Ngwea na kuangusha dua fupi.
Hata hivyo, baada ya yote hayo, kundi hilo la Wema na watu wake hatimaye walifanya dua fupi ya kumuombea malazi mema Albert Mangweha.
KUMBUKUMBU MUHIMU
Mangweha alikuwa msanii wa Bongo Fleva. Akiwa na miaka 31 alifariki dunia, Mei 28, 2013 nchini Afrika Kusini. Chanzo cha kifo chake inadaiwa ni matumizi yaliyopitiliza  ya madawa ya kulevya. Alizikwa Morogoro, Tanzania, Juni 6, 2013.

Kwa wale fans wa nguvu wa Wema Sepetu,hii kwa ajili yako… Ashoot video mpya na Van Vicker wa Ghana!


.
.
Staa wa kike wa Bongo Movie,Wema Sepetu yuko Ghana kwenye maandalizi ya movie mpya ‘Day After Death’ iliyomuhusisha kipenzi cha akinadada, staa wa filamu Van Vicker.
Kupitia kwenye instagram ya staa huyo wa Ghana alifafanunua zaidi kuhusu ujio wa filamu hiyo mpya aliyoshirikiana na Wema Sepetu
#MyNextBigThing I am excited abt our Ghana Tanzania collaboration. You finally landed. Today was day 1. good stuff. I love the way you are passionate abt what you want and u get it done. Enjoy workin with you. watch for Day After Death (D.A.D) #DayAfterDeath starring Wema@wemasepetu and me van vicker. I am directing again ya’ll and acting. it’s challenging but I love the challenge. Hey its my daughter’s j’dyl debut in films as an actor.Aliandika Van Vicker




KAJALA: NATAMANI KUPATANA NA WEMA

Stori: Imelda Mtema
SIKU chache baada ya mtangazaji Penniel Mungilwa ‘VJ Penny’ kupatana na Beutiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu, mwigizaji Kajala Masanja ‘Kay’ naye ameibuka na kuweka bayana kuwa hata yeye yupo radhi na anatamani kupatana na Wema ambaye wameogelea kwenye bifu miezi kadhaa sasa.
Waigizaji wa filamu Bongo, Kajala Masanja ‘Kay’ na Wema Sepetu wakati wakiwa pamoja.
Kajala alifunguka hayo mara baada ya paparazi wetu kumuuliza kuhusiana na mtazamo wake juu ya Wema na Penny kupatana ndipo aliposema amefurahi mno na hata watu wengine watakuwa wamejifunza kitu kutokana na kupatana kwao.
Akizidi kushusha ‘vesi’ mbele ya kinasa sauti cha Risasi Jumamosi, Kajala alisema anaamini siku zote bifu zinarudisha nyuma maendeleo hivyo Wema kupatana na Penny ni jambo la busara kwani ni moja ya chachu ya kufanya mambo mengine yaendelee kwani hata yeye hapendezwi na mabifu.
Wema Sepetu akipozi.
“Hata mimi natamani kupatana na Wema. Mabifu ni mambo ya kitoto sana, kwa kweli nimefurahi sana kuona Penny na Wema wamepatana kwani ni marafiki wa siku nyingi sana na wanastahili ifike sehemu vitu viishe na maisha yaendelee kama kawaida,” alisema Kajala.
Alipoulizwa Kajala kama kweli yupo tayari kupatana na Wema na uwezekano huo upo, Kajala alisema muda wowote wanaweza kukaa na kumaliza tofauti zao.“Hata mimi siku si nyingi tutaweka mambo sawa kwa sababu bifu hazijengi, hazina maana hata kidogo ni kufanya mambo yasiende mbele tu, inabidi tubadilike,” alisema Kajala.
Kajala Masanja ‘Kay’ akipozi.
Wema na Kajala walikuwa mashosti wa damu lakini mwaka jana mwishoni waligombana huku chanzo kikitajwa kuwa ni kugombea mwanaume ambaye alifahamika kwa jina la CK.

WEMA SEPETU ACHAFUA HALI YA HEWA INSTAGRAM KWA KUPOSTI PICHA HIZI



 

KAMA NI KUZAA ZAENI NYIE: WEMA SEPETU AWAPASHA WANAOMWANDAMA AZAE MTOTO.



Wema Wema Sepetu ameamua kuwatolea uvivu baadhi ya watu wanaomtaka azae mtoto. Wema mwenye miaka 25 kwasasa amesema hana mpango wa kuzaa kwa muda huu pengine kwakuwa umri wake bado sio mkubwa ni wa msichana wa kawaida. Wema amesema.................. "Okay... Lets get things straight here.... See that doggie up there... You all see her....? that is my bebi.... since i don't have a bebi... Huyo ndo mtoto wangu... Basi sasa nitapopost halafu nisikie kuzaa naku-block fasta... Mshaniona sizai basi ndo mjue sizai... Akha...!! Zaa zaa... If u have a child i'm happy for you... Na wish u thea best... I don't... Ndo Mungu alivyonipangia... So please hey.... Watakaozaa all da best... Walio na mipango ya kuzaa hongereni... Mimi sina ... I'm done... Vanilla ndo bebi wangu kipenzi na nampenda kuliko.... Na wale wa subhannah llah pia nisiwaone... This is getting too personal sasa..."

  

MAMA WEMA AFANYA SHEREHE

CHEREKO chereko! Siku chache baada ya supastaa ‘grade one’ wa sinema za Bongo, Wema Sepetu ‘madam’ kummwaga King of Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, mama mzazi wa mwigizaji huyo, Mariam Sepetu ameangusha sherehe ya nguvu kama ishara ya kuonesha ‘amekunwa’ na tukio hilo, Ijumaa Wikienda linashuka nayo mstari kwa mstari.
Supastaa ‘grade one’ wa sinema za Bongo, Wema Sepetu ‘madam’ akipozi.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, kutokana na mama huyo kutobariki uchumba wa mwanaye na Diamond ambaye pia anajulikana kwa jina la Dangote kwa muda mrefu, habari za uchumba huo kuvunjika zilipochapishwa kwenye Gazeti la Ijumaa ‘Kubwa’ toleo lililopita, moyo wake ulijawa na furaha.
“Mama Wema alichukizwa kwa kiasi kikubwa na mapenzi ya wawili hao kutokana na kile alichoamini kuwa, Diamond hakuwa na mapenzi ya dhati kwa mwanaye zaidi ya kutegemea nyota yake impe mafanikio ndiyo maana akafanya pati hiyo fupi nyumbani kwake Sinza-Mori, Dar,” kilisema chanzo hicho.
Wema Sepetu ‘madam’ akifurahi na mama yake, Mariam Sepetu
SHEREHE ILIVYOKUWA
Chanzo hicho kilizidi kumwaga unga kwamba, sherehe hiyo ilikuwa ni ya aina yake kwani mama Wema aliwaita mashosti zake, wakaandaa ‘menu’ ya ukweli kabisa, wakasherehekea lakini bahati mbaya Wema hakuhudhuria.
“Wema hakuweza kuhudhuria sherehe hiyo kutokana na kubanwa na majukumu mengine. Bi mkubwa aliwaita marafiki zake, wakafungua shampeni, wakala, wakanywa na kucheza muziki kufurahia Dangote kupigwa chini,” kilisema chanzo hicho.
Dangote wakati akiwa na Penniel Mungilwa ‘Penny’
MAMA NA CHUKI YA MUDA MREFU
Chanzo hicho kilizidi kumwaga ubuyu motomoto kuwa, mama Wema alipiga cherekochereko za kutosha siku hiyo kwani alikuwa akimchukia Diamond kwa muda mrefu.
“Mama Wema chuki zake kwa Diamond hazitaisha kamwe kwa kuwa hampendi tu kutokana na kuona mwanaye hasongi mbele kimaendeleo kama alivyo Diamond ambaye akiachana na Wema mambo yake hayamwendei vizuri kama anavyokuwa na mwanaye.”
Diamond wakati akiwa na Jokate Mwegelo.
MAMA WEMA ANENA
Baada ya wanahabari wetu kunasa maelezo hayo ya chanzo, walimvutia waya mama Wema ambaye alikiri kufanya sherehe fupi baada ya mwanaye kummwaga Diamond.
“Mimi naona huu ndiyo mwisho wa Wema na Diamond na siku zote nasema hakuna uhusiano ukadumu bila baraka za wazazi, niseme tu, sitaki kumuona ndugu yeyote wa Diamond kwangu, kama mahari wakatoe kwa Penny siyo kwa mwanangu,” alisema mama Wema.
Wema Sepetu,'Madam' akiwa na Diamond Platinumz.
TUJIKUMBUSHE
Kumwagana kwa Wema na Diamond safari hii, ni mara ya nne. Awali walimwagana, wakarudiana, wakamwagana tena, Diamond akatua kwa Jokate Mwegelo, wakarudiana tena na Wema, wakaja mwagana tena, Diamond akatambaa na Penniel Mungilwa ‘Penny’, wakamwagana, karudiana na Wema, sasa  wamemwagana tena.

Wema Sepetu: Najuta Kuwa Maarufu


‘BEAUTIFUL Onyinye’, WEMA Isaack Sepetu ‘Madame’ ametoa ya moyoni na kufichua kwamba maisha yake ya umaarufu anayoishi yanamtesa kwa asilimia 40.
Pamoja na mateso hayo, staa huyo wa filamu alisema anafurahia maisha yake kama mtu maarufu ikiwamo na kuandikwa na vyombo vya habari mara kwa mara.
“Kuna wakati najutia kuwa maarufu kwa asilimia kama 40 hivi lakini nashukuru kwani kwa asilimia 60 nayafurahia maisha yangu.
 
“Ukiwa nyota kuna changamoto nyingi sana, kuna wakati mtu anaweza kukuandika habari inayokufanya ushindwe hata kutoka nje na kubaki ndani tu,”alisema.
Wema Sepetu
Wema alisema kuna wakati huwa anatamani asingekuwa maarufu kwani akifanya kitu kidogo hata kama ni cha kawaida lakini hupokelewa kama habari kubwa na kuongelewa sana.
“Lakini katika maisha kama haya sina cha kufanya japo kuna mambo ambayo huniumiza na najitahidi sana kuvumilia,” alisema.
   

NI SHEEDAH 'WEMA, AUNTY HUSAGANA'

Stori: Musa Mateja na Imelda Mtema
Ni sheedah! Pamoja na kukanusha kwa kutumia nguvu kubwa, nyuma ya ushosti wa mastaa grade one wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na Aunty Ezekiel kuna siri nzito ikidaiwa kwamba wawili hao husagana.Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na Aunty Ezekiel wakidendeka hadhalani.
TUKIO BICHI
Madai hayo ya muda mrefu huku wenyewe wakisisitiza si ya kweli, yameibuka upya juzikati baada ya warembo hao kuonesha mahaba niue au nikongorowe kisha ‘kudendeka’ hadharani na kusababisha mwandani wa Wema, Nasibu Abdul ‘Diamond’ kukasirika na kuondoka eneo la tukio akiambatana na timu yake ya Wasafi Classic Baby (WCB).
ILIKUWAJE? Tukio hilo lililoshuhudiwa na wanahabari wetu lilijiri usiku wa kuamkia Oktoba 28, mwaka huu ndani ya Mgahawa wa Rodizio, Masaki jijini Dar ambapo Aunty alikuwa akisherehekea siku ya yake ya kuzaliwa ‘bethidei’.
WEMA ATOKEA DUBAI
Shughuli hiyo ilitawaliwa na matukio baada ya Wema kuwasili ukumbini hapo akitokea nchini China kupitia Dubai alikokwenda hivi karibuni kwa biashara binafsi ikidaiwa kwamba amerejea na mkwanja wa kutosha.
Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na Aunty Ezekiel wakifurahiya jambo.
Wema alitinga ukumbini hapo saa 7:15 usiku na kuwakuta wadau wakiendelea na sherehe hiyo ambapo mara tu baada ya kufika alikumbatiana kimahaba na  Aunty zoezi lililochukua dakika kadhaa wakiwa wamenasiana huku wakifunika nyuso zao kwa zile nywele nyingi za Wema hivyo kilichoendelea humo ndani hakikujulikana. Walipojifunua kwenye nywele ndipo ikabaini kwamba kumbe walikuwa ‘wakidendeka’ bila kujali wingi wa kamera.
WASHUTUMIWA
“Mungu wangu, leo mambo hadharani. Mbona ni sheedah? Yaani wanadendeka hadharani! Kwa vyovyote vile Wema na Aunty husagana,” alisikika mmoja wa waalikwa.
Staa wa Filamu Bongo, Aunt Ezekiel akikata keki  ya bethidei yake ndani ya Ukumbi uliyopo kwenye   Mgahawa wa Rodizio Masaki.
Mmoja wa waigizaji chipukizi alidakia: “Yaani utadhani wapenzi kabisa maana kila mmoja anaonesha hisia za kumisiana. Hawaogopi kuambiwa wanasagana? Haya bwana, yetu macho maana leo tutaona mengi. Vitendo kama hivi ni vya kulaaniwa vikali na kuwakumbusha kwamba wao ni kioo cha jamii.”
DIAMOND AKASIRIKA, AONDOKA
Kufuatia  hali hiyo, Diamond alionekana kukasirika na kushindwa kuvumilia hivyo aliamua kuwaacha wajinafasi kwa kuondoka ukumbini akiwa ameambatana na timu yake. Waalikwa waliokuwa ndani ya ukumbi huo waliendelea kupigwa butwaa na kitendo hicho hasa Diamond alipoamua kusepa huku nyuma Wema na Aunty wakibaki huru na kuendelea kufanyiana mambo ya kimahaba mara nyingine wakati wakilishana keki kwa staili ya njiwa.
Diamond na Aunt Ezekiel wakijadiliana jambo muda mfupi baada ya kuwasili ukumbini hapo.
AMANI LAMVAA AUNTY
Baada ya kuona hali hiyo, paparazi wa Amani aliyekuwa ukumbini hapo alimvaa Aunty na kumuuliza kwa nini ameamua kuonesha hali hiyo mbele ya kadamnasi ambapo alijibu hakuna mambo ya usagaji. Alisema hali hiyo ilitokea tu maana yeye na Wema ni marafiki ambao wameshapitiliza hivyo wamejikuta wakiwa kwenye hali hiyo bila wao kuona kama ni tatizo. “Kwani nani asiyejua kama mimi na Wema ni marafiki, suala la kukisiana ni jambo la kawaida kwetu.
Shilole (kulia), akilishwa keki na Aunt Ezekiel.
MAMA LA MAMA  
Kwa upande wake mama la mama Wema aliishia kusema kuwa alimmisi sana shoga’ke na hakuna jambo la ajabu ambalo amelifanya juu yake maana wao ni marafiki kama marafiki wengine.
TUJIKUMBUSHE
Kwa muda mrefu Wema na Aunty wamekuwa marafiki ambapo kila mmoja hulala kwa mwenzake tena kitanda kimoja tangu Wema alipotofautiana na Kajala Masanja ambaye naye aliwahi kuhusishwa na masula ya usagaji na staa huyo mkubwa asiyechuja.

WEMA AZUA KIZAAZAA CHINA

Na Mwandishi wetu
KUONESHA ameguswa, Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ alizua kizaazaa cha aina yake alipomtembelea mwanamitindo Jacqueline Fitizpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ gerezani nchini China.
Tukio hilo lilitokea juzikati kwenye gereza lililopo Mji wa Macau ambapo Wema aliambatana na meneja wake, Martin Kadinda pamoja na shemeji yake, Petit Man.
Beautiful Onyinye, Wema Sepetu ‘Madam’ akiwa na meneja wake, Martin Kadinda.
Chanzo kilicho karibu na Wema kimeeleza kuwa, Wema alipofika na kuona mazingira ya upweke ambayo Jack anaishi, aliwaza kwa muda na kuzungumza maneno kama mtu aliyechanganyikiwa hivyo kuwatia hofu Martin na Petit.
Mwanamitindo Jacqueline Fitizpatrick Cliff ‘Jack Patrick’ wakati akiwa huru Bongo.
“Ilikuwa mshikemshike, alimmis sana Jack sasa alipomuona na mazingira yale ya upweke ndicho kilichomchanganya Wema lakini baadaye kina Martin walimrudisha kimawazo na hatimaye akawa sawa,” kilisema chanzo hicho na kuongeza:
Kete za madawa ya kulevya zilizowahi kunaswa.
“Hata hivyo, Wema amesema mazingira ya kule ndani siyo mabaya lakini kilichomuumiza yeye ni upweke ambao anao na watu wanaomzunguka.”
Jack alikamatwa Desemba 19, mwaka jana akiwa amebeba madawa ya kulevya aina ya Heroin yenye uzito wa kilo 1.1 katika Uwanja wa Ndege wa Macau akitokea jijini Bangkok nchini Thailand kuelekea Guangzhou, Mji Mkuu wa Jimbo la Guangdong Kusini mwa China.
Agosti, mwaka huu Jack Patrick ilielezwa kuwa alihukumiwa kifungo cha miaka sita jela huku kukiwa na uwezekano wa kupunguziwa adhabu endapo ataonesha utiifu gerezani.
Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top