Habari Kali
Loading...

Olamide karudi tena kwenye headlines na hii nyingine ‘Eyan Mayweather’…(Video)

Moja ya mastaa wanaofanya vyema katika industry ya muziki Nigeria ni pamoja na Olamide ambaye tayari nyimbo zake nyingi zikiwemo alizowashirikisha mastaa mbalimbali zimefanya vizuri.
Olamide ameamua kuja na video yake mpya ya single yake ya Eyan Mayweather’ iliyofanyika jijini Lagos.
Nakukaribisha kuitazama hapa


BURUDANI YA NGUVU TOKA KWA YAMOTO BAND SIKU YA MSANII

Kundi la Yamoto Band wakitoa burudani Siku ya Msanii usiku wa leo Mlimani City jijini Dar.
(PICHA: MUSA MATEJA/GPL)

RED CARPET YA MISS TANZANIA 2014 MLIMANI CITY

Miss Tanga ambaye pia ni Miss Reds 2007, Victoria Martin.
Mtangazaji wa Kipindi cha Bongo Beats cha Star TV, Sauda Mwilima.
Mtangazaji wa Channel Ten, TJ akiwa katika pozi.
Msanii wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz akiwa katika pozi.
Mmoja ya washiriki wa Miss Moshi, Glory akiwa katika pozi.
Glory akiwa na mama yake.
Mrembo akiwa katika Red Carpet.
Miss Kanda ya ziwa, Rashida Wanjara.
Miss Sinza, Husna Maulid.
Warembo wakiwa katika pozi.
Wadau wa Redds Miss Tanzania 2014.
Miss Tanzania namba tatu 2003/04, Nargis Mohamed akiwa katika pozi.
Msanii wa Bongo Fleva, Msami Baby.

OFFICIAL VIDEO: PAM DAFFA - NIMEMPATA FT. MESEN SELEKTA

MISS TANZANIA 2014 ACHA KABISA

Acha kabisa! Fainali ya lile shindano kubwa la mrembo wa Miss Tanzania 2014 limechukua nafasi usiku wa kuamkia jana, Jumapili ambapo Ijumaa Wikienda lilikuwepo ndani ya eneo la tukio kukukusanyia matukio yote yaliyojiri mbele na nyuma ya pazia hivyo lina full story.
Warembo 30 walioshiriki kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, wakionesha shoo ya kufa mtu.
WAREMBO 30
Baada ya Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania na Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga ‘Anko’ kukaribisha wageni waalikwa, warembo 30 walioshiriki kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania, walionesha shoo ya kufa mtu kupitia kwa msanii wa nyimbo za asili, Wanne Star.
Vanessa Mdee akifanya makamuzi jukwaani
VANESSA AFUNIKA
Kabla ya mambo mengine kuendelea, Vanessa Mdee alifunika kwa bonge la shoo alilokamua , akisindikizwa na wacheza shoo wake wawili ambao walikamua ile mbaya.
MVUTO KWENYE PICHA
Aliyeibuka kidedea kwenye kipengele hicho ni Evelyn Bassah huku Kipengele cha Top Model, mrembo Jihan Dimach akijitwalia taji.
Warembo walifanikiwa kuingia Top Five.
KIPAJI
Katika Kipengele cha Miss Talent (kipaji), taji lilikwenda kwa Nicole Sarakikya, Elizabeth Tarimo akaibuka kidedea kwenye Kipengele cha mwanamichezo mwanamke (Sports woman) huku Miss Personality ikitwaliwa na Salama Saleh.
KIFUTA JASHO
Baada ya kuenguliwa warembo 15, wale top 15 waliosalia walilamba Sh. laki saba kila mmoja kama kifuta jasho.
TOP 5
Washiriki waliofanikiwa kuingia kwenye Tano Bora ni Jihan Dimach, Siti Mtemvu, Dorice Mollel, Nasreen Abdul na Lilian Kamazima.
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia shoo.
WAVALISHWA KAMA NDEGE TAUSI
Bila shaka unawajua ndege tausi hasa wale wanaoonekana pale Ikulu ya Magogoni. Warembo hao walioingia Top 5 walikuwa wamevalishwa kama ndege huyo isipokuwa rangi kwa namna walivyoonekana jukwaani.
MREMBO AMWAGA KIFARANSA
Wakati wa kipindi cha maswali na majibu, mrembo Siti Mtemvu aliwaacha watu midomo wazi aliposema atajibu kwa Kiingereza lakini baada ya kumaliza kumwaga ung’eng’e, akamalizia kwa kutema Kifaransa.
Meza ya majaji ikijipanga kutoa uamuzi wa mwisho katika kinyang'anyiro hicho.
MWINGINE ACHEMKA
Naye mrembo mwingine, Nasreen Abdul alijikuta akichemka kujibu maswali hivyo kuzomewa hasa pale alipochanganya kati ya maneno tourism (utalii) aliloulizwa na terrorism (ugaidi).
JIHAN ALA SHANGWE
Kwenye ‘segmenti’ ya maswali na majibu, mrembo Jihan alijikuta akipokea shangwe la kufa mtu kwa kujibu vizuri kwa ung’eng’e.
Siti Mtemvu (Miss Tanzania 2014 ) akiwa na anyedaiwa ni baba yake, Mbunge wa Temeke (CCM), Abbas Mtemvu.
VITUKO VYATAWALA
Vituko vilivyojiri vilikuwa vingi kwa mfano katika shoo ya msanii Vanessa Mdee aliyetumbuiza katika shindano hilo, alijikuta akiachia  ‘nido’ moja nje wakati akicheza na kuchafua hali ya utulivu, akaibua zomeazomea ya ‘weweeeee’.
nyuma ya pazia
Kituko kingine ni cha mtangazaji maarufu Bongo, Gardner G. Habash kutinga ukumbini akiwa ameongozana na kale kabinti ambako katika siku za hivi karibuni, amekuwa akionekana akiwa beneti nako bila Lady Jaydee kujua.
Ommy Dimpoz akipiga shoo katika fainali hizo
Baada ya shoo kali ya Ommy Dimpoz, washiriki walioingia fainali, walipanda tena jukwaani ambapo Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga naye  alipanda jukwaani na kuanza kuwatangaza washindi, kuanzia namba tano mpaka namba moja.
Nasreem Abdul alishika nafasi ya tano, nafasi ya nne ikaenda kwa  Dorice Mollel.
TOP THREE
Jihan Dimach alitangazwa kuwa mshindi wa tatu (second runner up) wakati Lilian Kamazima, alishika nafasi ya pili (first runner up).
Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania na Mkurugenzi wa Lino International, Hashim Lundenga ‘Anko' (kushoto) akisimamia shoo.
Nafasi ya kwanza, ilishikwa na Siti Mtemvu, mrembo kutoka Temeke ambaye alitawazwa kuwa Miss Tanzania 2014 na kuvalishwa taji na Miss Tanzania 2013, Happiness Watimanya.
Pia Siti alijishindia shilingi milioni 18 za Kitanzania kama zawadi kwa ajili ya mshindi wa kwanza huku Lilian na akiondoka na shilingi milioni 6 za Kitanzania na Jihan akiambulia milioni 4.2.
MSHINDI ALIJULIKANA MAPEMA?
Swali kubwa ambalo wadau wengi wa mashindano ya umiss Tanzania walijiuliza usiku huo ni kwamba, je, mshindi alijulikana mapema?
Mashabiki wakipigia debe na kutoa sapoti kwa Mrembo Siti Mtemvu katika kinyang'anyiro hicho.
Viashiria vya mapema vilionesha kwamba, Siti ambaye inadaiwa ni mtoto wa Mbunge wa Temeke (CCM), Abbas Mtemvu angeibuka mshindi kutokana na jinsi alivyokuwa akishangiliwa kwa nguvu huku wapambe wake wakiinua vipeperushi vyenye picha ya mshiriki huyo, hali ambayo haikuwepo kwa wenzake.
Waandishi: Issa Mnally, Gabriel Ng’osha na Musa Mateja

SITTI MTEMVU ALIVYOTWAA TAJI LA MISS TANZANIA 2014


MREMBO Sitti Mtemvu aliyekuwa Miss Temeke 2014, Oktoba 11, 2014 aliibuka kidedea katika fainali za shindano la Miss Tanzania 2014 na kujinyakulia taji hilo sambamba na shilingi milioni 18.
Katika shindano hilo lililofanyika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar, nafasi ya pili ilikwenda kwa Lilian Kamazima ambaye alijishindia shilingi milioni 6 huku nafasi ya tatu ikichukuliwa na Jihan Dimachk.
Dorice Mollel alishika nafasi ya nne wakati Nasreen Abdul akichukua nafasi ya tano.

MATUKIO YA REDDS MISS TANZANIA 2014 MLIMANI CITY DAR

 
Pichani ni Washiriki waliochaguliwa kuingia kwenye hatua ya tano bora katika shindano la Redds Miss Tanzania 2014 linaloendelea hivi sasa ndani ya ukumbi wa Mlimani City, jijini Dar.
Mmoja wa Washiriki waliongia katika nafasi ya tanno bora shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakijibu maswali mbalimbali.
Msanii wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz akitumbuiza jukwaani akiwa na Vanessa Mdee mbele ya wageni waalikwa (hawapo pichani),waliofika kushuhudia shindano hilo.
Msanii wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee 'V-Money' akitumbuiza kwenye shindano la kumsaka mshindi wa Redds Miss Tanzania 2014,yanayofanyika usiku huu ndani ya moja ya ukumbi wa Mlimani, jijini Dar.
Washiriki wa Redds Miss Tanzania 2014 wapatao 15 mara baada ya kuchujwa.
Baadahi ya Wageni waalikwa wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri kwenye shindano hilo la kumsaka Kinara wa Redds Miss Tanzania 2014.
Washiriki wa Shindano la Redds Miss Tanzania 2014 wakicheza moja ya onesho lao la ufunguzi wa shindano hilo,ambapo mshindi atatangazwa usiku huu na kujinyakulia kiasi cha shilingi miloni 18 taslim.

Serengeti Fiesta Dar kuonekana live mtandaoni!




Waandaji wa tamasha la Serengeti Fiesta kwa kushirikiana na Clouds TV wametangaza kurusha mtandaoni moja kwa moja sehemu ya matangazo ya tamasha la Serengeti Fiesta 2014 ambalo mwaka huu litashereheshwa na mwanamuziki kutoka Marekani, T.I ambaye pia ni mshindi wa tuzo ya Grammy.

Tamasha hilo litafanyika katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam tarehe 18 mwezi wa kumi mwaka 2014
 
Kwa mujibu wa TanzaniaBox.com baadhi ya vipande vya sehemu ya tamasha la Serengeti Fiesta na matukio maalumu ya nyuma ya pazia yatarushwa moja kwa moja na yataweza kutazamwa popote pale duniani kwa kifaa chochote kilichounganishwa na mtandao wa intaneti kama simu zenye uwezo wa kuonyesha video, komputa ndogo, komputa kubwa pamoja na TV zilizounganishwa na mtandao.
 

Mashabiki wa Serengeti Fiesta duniani wataweza pia kufuatilia moja kwa moja pale wasanii wakubwa wa Bongo Flava kama Diamond, Ali Kiba, Ney wa Mitego na Vanessa Mdee pamoja na wasanii wengine wa kimataifa kama Waje, Victoria Kimani, Ash Hamman pamoja na mkali kutoka Marekani T.I wakitoa burudani.
   

KATUNI


LAVEDA AFUNIKA UFUNGUZI WA BIG BROTHER HOTSHOTS


Irene 'Laveda' akionyesha ufundi wa kutumia saxophone wakati akitoa shoo kwenye ufunguzi wa Big Brother Hotshots.
MSHIRIKI wa shinadano la Big Brother Hotshots kutoka Tanzania, Irene 'Laveda' amefunika vilivyo katika shoo ya ufunguzi wa shindano hilo usiku huu nchini Afrka Kusini.
Laveda ameongoza kwa kura zilizopigwa na watu waliokuwa mjengoni akipata asilimia 85 kutokana na shoo yake kali aliyotoa akicharaza vilivyo saxophone na kuwafunika washiriki wengine 25 kutoka mataifa mengine ya Afrika.
Kwa ushindi huo, Laveda hatakuwemo katika orodha ya washiriki watakaopigiwa kura kwa ajili ya kutolewa mjengoni kuanzia wiki ijayo.

SERENGETI FIESTA 2014 YAFUNIKA DODOMA

Msanii wa Bongo Fleva, Baba Levo akitumbuiza kwa staili yake kwenye jukwaa la Serengeti Fiesta 2014 Dodoma usiku wa kuamkia leo.
Mo Music akitoa burudani kwa wakzi wa Dodoma waliyofulika kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 ndani ya Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma.
Msanii zao la Serengeti Super Nyota G-Lucky akifanya makamuzi ndani ya uwanja wa Jamhuri Dodoma.
Y-Tony akiwajibika kwenye tamasha la Serengeti Fiesta lililokuwa likifanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri Dodoma.
Chipukizi wa Bongo Fleva, Baraka Da Prince akiwajibika jukwaani.
Msanii zao la nyumba ya kukuza vipaji Tanzania (THT), Kadja Maumivu akipagawisha kwenye jukwaa la Serengeti Fiesta 2014, usiku wa kuamkia leo.
Young Killer akimwaga mistari ya Hip Hop kwa mashabiki waliyojitokeza kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2014 lililokuwa likifanyika ndani ya Uwanja wa Jamhuri  mjini Dodoma.
Mr Blue akifanya yake jukwaani.
Recho akiimba jukwaani huku mmoja wa wanenguaji wake akiwajibika kwa staili kali.
Mkongwe wa Bongo Fleva, Dully Sykes akipagawisha jukwaani.
Vanessa Mdee katikati akipagawisha kwenye jukwaa la Serengeti Fiesta ndani ya Uwanja wa Jamhuri Dodoma.
Jux akikamua jukwaani.
(PICHA NA MUSA MATEJA/GPL, DODOMA)
Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top