
Mzee Edward Lowassa amesema anajiandaa kwa uchaguzi 2020, mafuriko yaikumba Mwanza huku mtoto mmoja akifariki…. Tundu Lissu asema viatu vya nafasi ya Dk. Slaa ni vikubwa CHADEMA, CUF wasema wanaheshimu mazungumzo ndio maana wako kimya kuhusu ishu ya Zanzibar.
Jeshi la Polisi latoa
mbinu tano za kuepukana na wizi watu wanapotoka kuchukua fedha Benki,
Serikali imesema itawanyang’anya viwanda na mashamba kwa walioshindwa
kuviendeleza.
Askari Polisi mmoja na watu wengine watatu wafikishwa Mahakamani Dar kwa tuhuma za wizi wa magari, wananchi wa Manyara wampiga
Askari na kumpora bunduki kwenye mnada, elimu ya bure ni kaa la moto
Dar, walimu wakosekana na vifaa vyaibiwa.. Serikali yaagiza watuhumiwa
wa kesi za kuozeshwa mtoto wa miaka 13 wachukuliwe hatua.
Pingamizi la Serikali kupinga kesi ya David Kafulila latupiliwa mbali Mahakamani Tabora.
Stori zote ziko kwenye uchambuzi wa sauti pia kutoka Powerbreakfast Clouds FM.