Habari Kali
Loading...

Adele anafunga mwaka wa 2015 na haya mambo sita: Umaarufu, Album mpya na mengine!

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
Adele ndiye staa wa muziki anayefunga mwaka wa 2015 kwenye headlines za burudani Marekani na dunia nzima akiwa ameuza zaidi ya nakala milion 5 za single yake mpya ‘Hello’ huku video yake ikiwa imegusa watazamaji milion 700 kwenye mtandao wa YouTUBE! Ujio mpya wa Adele kwenye kurasa za burudani umepokelewa kwa muamko mkubwa sana duniani.
TIME4
Nimekutana na interview ya Adele na jarida la TIME Magazine la Marekani na ndani yake staa huyo amegusia vitu vingi ikiwemo album yake mpya 25, social media pamoja na mauzo ya juu nchini Marekani.
TIME2
Hivi ni baadhi ya vitu alivyovigusia Adele na interview yake na TIME Magazine:
Mauzo ya nakala zaidi ya mamilioni Marekani: Inashangaza kidogo na kunishitua sana. Ukizingatia mimi hata sio Mmarekani. Labda wanafikiri nina undugu na Malkia…
TIME
Mtazamo wake kuhusu kuitwa ‘Brand’: Kila mtu analitumia neno hilo. Sipendi kuitwa ‘brand’ wananifanya nionekane kama aina fulani ya bidhaa au kama packet la kripsi… msanii ni package ya vitu vingi!
SATURDAY NIGHT LIVE -- "Matthew McConaughey" Episode 1689 -- Pictured: Musical guest Adele performs on November 21, 2015 -- (Photo by: Dana Edelson/NBC/NBCU Photo Bank via Getty Images)
Kwanini watu huupokea vizuri muziki wake: Uhalisia nilionao ni kwamba sioni aibu kuimba ukweli unaonigusa hata kama mimi ndio mwenye makosa. Kila mtu hufanya makosa. Watu wengi hujifanya wajasiri kwasababu wanaogopa kuonyesha udhaifu wao. Mimi najaribu kuimba nyimbo zinazogusa vitu vya ukweli kwa mashabiki wangu kwa  sababu kama mimi hata wao wanaumizwa na vitu mbalimali maishani japo natumaini pia nyimbo zangu zitaleta furaha kwenye maisha ya mashabiki wangu na sio huzuni na machungu“.
TIME7
Mitandao ya kijamii ina nafasi gani kwake: Napenda kuweka mambo yangu private… kuwa na privacy inakuwezesha kuandika nyimbo za ukweli utakaogusa watu, waupende au wasiupende bado utakuwa ukweli. Maisha yangu yamebadilika sana toka niachie ‘Hello’ na hiyo inanipa changamoto, hivyo siwezi kukaa kusubiria likes milioni na kwa picha moja… nitapata wapi muda wa kutunga nyimbo zitakazogusa watu? Huo sio uhalisia“.
TIME6
Maisha yake binafsi ya nyumbani yapoje: Nina maisha ya kawaida, nahisi watu wengi wangekuwa wanajua jinsi ambavyo maisha yangu ni ya kawaida wangeshangaa. Kama sina kazi zozote huwa nashinda tu nyumbani na familia yangu… ni muhimu kutokupagawa na hivi vitu, ni muhimu pia kukumbuka kuishi kama watu wengine wote wa kawaida.
TIME8
Kuhusu kufanya Collabo na wasanii wengine?: Album yangu 25 haina collabo yoyote lakini hiyo haimanishi hakutakuwa na collabo kwenye album yangu ijayo baada ya hii… zile tetesi za mimi kukataa kushirikiana na Beyonce hazikuwa za ukweli, sikuweza kufanya collabo na mtu kwenye album hii kwa sababu nilikuwa nashindwa kugawa muda na kufanya maamuzi ya kufanya kazi na nani...”

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top