Habari Kali
Loading...

Maskini :Mtoto Mchanga Apigwa na Mchi Kichwani Dodoma

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== > Mtoto mchanga mwenye umri wa mwezi mmoja, Yadiko Chigoda amelazwa katika Hospital ya Benjamini Mkapa Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma baada ya kupigwa na mchi kichwani na baba yake mzazi na kumsababishia maumivu makali.
Akizungumza mama mzazi wa mtoto huyo, Carolina Mnyawami ambaye ni mkazi wa kijiji cha Mingui kata ya Lumuma Wilayani Mpwapwa amesema tukio hilo limetokea leo majira ya saa 4 asubuhi ambapo mume wake aliyefahamika kwa jina la Fabian Chigoda alikuwa anapigana na kaka yake hivyo aliamua kuwaamulia ugomvi wao.
DODOMA
Amesema katika ugomvi huo walikuwa wanapigana na fimbo, hivyo alipowanyang’anya fimbo hiyo ili wasiendelee kupigana ndipo (Chigoda) alipoamua kuchukua mchi ili ampige nao mkewe kichwani lakini alikwepa na alipourusha ndipo ulipompata mtoto huyo kichwani.
“Nilipowanyang’anya fimbo ili wasiendelee kupigana, mume wangu aliokota mchi na kunirushia kichwani.. kwa bahati nzuri niliuona mchi huo na kukwepa ili usinipige ndipo ulipompiga kichwani mwanangu niliyekuwa nimembeba mgongoni,” amesema Carolina.
Ameongeza kuwa, “Baada ya kuona kuwa amempiga mtoto alikimbia na hajulikani alipo mpaka sasa.”
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Said Mawji amethibitisha kumpokea mtoto huyo na kwamba hivi sasa mtoto huyo anaendelea kupata tiba na uchunguzi zaidi wa afya yake.
“Ameumia sana kichwani lakini bado tunampatia tiba na uchunguzi zaidi kwenye fuvu la kichwa, kwani inaonekana kama vile limepasuka,” amesema Dk, Mawaji.
Hata hivyo amesema kuwa wanafanya mpango wa kumpa rufaa mtoto huyo ili aweze kwenda kutibiwa katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Mingui, Mwingwa Udoba amesema chanzo cha tukio hilo ni ugomvi wa kifamilia na kwamba bado wanamtafuta baba mzazi wa mtoto huyo kwa kuwa alikimbia baada ya tukio hilo.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime alipotafutwa kuzungumzia tukio hilo simu yake ilipokelewa na mtu aliyesema kuwa Kamanda alikuwa kwenye kikao cha kazi.

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top