WAKATI
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiendelea na msimamo wa uwapo wa
mfumo wa Serikali tatu, Bunge Maalumu la Katiba limeanza kujadili baadhi
ya sura ambazo ziliachwa na iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa
ajili ya Katiba ya Tanganyika.
Akizungumza
na waandishi wa habari mjini hapa Dodoma, Mwenyekiti wa Bunge hilo,
Samuel Sitta, alisema sura hizo ni pamoja na ile ya Serikali za Mitaa na
suala la ardhi.
Kwa
mujibu wa iliyokuwa Tume ya Warioba, maeneo hayo yaliachwa kwa ajili ya
Serikali ya Tanganyika. Sitta alisema kuwa suala la Serikali za Mitaa
liliwasilishwa kwenye Kamati ya Uongozi wa Bunge hilo na Waziri wa
Katiba na Sheria, Dk. Asha-Rose Migiro, ambaye alilitoa kwa wajumbe wa
Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT).
Alisema
waziri huyo aliwasilisha andiko la Jaji Warioba kuhusu ardhi, maliasili
na rasilimali za taifa lililokuwa limeandaliwa kwa ajili ya Katiba ya
Tanganyika.
“Tumechukua hayo ya tume ili kuendelea kuiboresha rasimu yetu hii tuliyonayo,” alisema.
Alisema kuwa pendekezo jingine kutoka kwa wajumbe wa Bunge hilo ni malengo ya maendeleo, uchumi na jamii.
“Tunataka Serikali isione kuwa kazi yake ni kuongoza watu tu, wajue kwamba wanatakiwa kuhakikisha wanawaendeleza watu kiuchumi,” alisema Sitta.
Katika
hatua nyingine, alisema kuwa Kamati ya Uongozi imeunda kamati ndogo ya
watu 10 kupitia suala la Mahakama ya Kadhi, uraia pacha na muundo wa
Bunge.
Alisema
kuwa kamati hiyo inaongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia
Suluhu na ina wajumbe watano kutoka Zanzibar na watano kutoka Bara.
Sitta alisema kuwa kamati zote zinatarajiwa kumaliza kazi zake Agosti 27, na Septemba 2 wajumbe wataanza kujadili sura zote.
Alisema
pamoja na hali hiyo, wajumbe wamependekeza Katiba mpya itambue haki za
walaji ili iwapo mtu akinunua kitu kibovu imlinde.
“Baada ya kazi ya Bunge kwisha, tutakuwa na Katiba bora Mashariki na Kusini mwa Jangwa la Sahara, Katiba ya viwango kabisa,” alisema Sitta.
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >



