Habari Kali
Loading...

Mbio za Urais CCM: Benard Membe Ataka Jina la Edward Lowassa Lisikatwe.......Atamani Akutane Naye Tatu Bora Ili Amwonyeshe Uwezo Wake

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, ambaye jina lake linatajwa kutaka kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, anaelezwa kutamani kuingia katika hatua za mwisho za kinyang’anyiro hicho na Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa.
 
Vyanzo vya habari ndani CCM vinasema kwamba Membe amekua akionyesha kutamani kuingia katika hatua ya 'tatu bora' pamoja na Lowassa ili aonyeshe uwezo wake ndani ya chama hicho, tofauti na wapinzani wake wanaodai hana nguvu kisiasa na hawezi kushindana na Lowassa ndani ya chama.
 
"Membe anatamani sana kama akigombea aingie na Lowassa katika hatua ya mwisho maana anatamani aonyeshe uwezo wake, kama alivyowaonyesha katika uchaguzi wa kuingia NEC (Halmashauri Kuu ya CCM) mwaka 2012, ambao walimpiga vita na kutumia fedha nyingi lakini akapata kura za kutosha bila kampeni ya nguvu na kuwatia aibu," anasema mtoa habari huyo ndani ya CCM.
 
Katika uchaguzi huo wa mwaka 2012 ambao Lowassa hakugombea katika ngazi ya Taifa na badala yake aligombea kupitia Wilaya ya Monduli, Membe alipata kura 1,455 ikiwa ni asilimia 74 ya wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM pamoja na kupigwa vita na wanasiasa ili asipite na kuingia NEC.
 
Hata hivyo, habari za ndani ya CCM zinaeleza kwamba kupita kwa Lowassa ni mtihani mgumu kwa chama hicho kutokana na ukiukwaji wa maadili anaodaiwa kuufanya mwanasiasa huyo ambaye ni Mbunge wa Monduli.
 
Baadhi ya ukiukwaji wa maadili anaodaiwa kuufanya Lowassa ni pamoja na kufanya kampeni wakati akiwa katika adhabu anayotumikia na wenzake watano, akiwamo Membe, ambao walifungiwa kwa miezi 12.
 
Wengine katika orodha hiyo ni aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba, Waziri Mkuu wa zamani, Frederick Sumaye na Waziri wa Kilimo na Chakula, Steven Wasira.
 
Juhudi za kumpata Lowassa kutoa maoni yake kuhusu matamanio hayo ya Membe hazikufanikiwa kwa vile inaelezwa kwamba yuko mapumziko visiwani Zanzibar ambako amepumzika na pililapilika za kisiasa.
 
Hata hivyo, Msemaji wa Lowassa, Abubakari Liongo, alisema ingawa ingekuwa vema zaidi kama bosi wake huyo angejibu mwenyewe kuhusu jambo hilo, kwa sasa bado ni mapema kuzungumza kuhusu kinyang’anyiro hicho.
 
“Hili si suala la kisera na limekaa kibinafsi na hivyo nadhani Mzee (Lowassa) mwenyewe angeweza kuzungumza. Hata hivyo, akizungumza kuhusu hilo inaweza kutafsiriwa kwamba anapiga kampeni na hivyo naona ni mapema kwa sasa kusema lolote,” alisema.
 
Lakini wakati msemaji huyo akibainisha hayo, tayari baadhi ya wanasiasa walioko kwenye kambi hiyo ya Lowassa wamekuwa wakijigamba kuwa na nguvu ndani ya chama hicho, hasa katika Halmashauri Kuu (NEC) na Mkutano Mkuu, hali inayonogesha mpambano huo wa fainali ambao Membe anatajwa kuutamani kama atatangaza kuwania na kisha kuteuliwa.
 
Hofu ya kwamba Lowassa anaweza kukatwa jina lake na vikao vya CCM inachangiwa na mambo mengine kadhaa anayotajwa kuyafanya kiasi cha kukiuka masharti ya adhabu aliyopewa sambamba na makada wenzake hao ndani ya CCM.
 
Miongoni mwa matukio yaliyosababisha hadi Lowassa kuonywa na Sekretariati ya CCM kupitia kwa Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye ni kuandaa makundi kadhaa yaliyokuwa yakifika nyumbani kwake, Dodoma na Monduli (Arusha), kwa ajili ya kile kilichokuwa kikielezwa ni kumwomba (kumshawishi) agombee urais.
 
Tayari kundi la Lowassa limekwishaweka bayana kwamba ‘ushawishi’ huo ni mwitikio wa wito alioutoa Rais Jakaya Kikwete, Songea, mkoani Ruvuma katika maadhimisho ya miaka 38 ya kuzaliwa kwa CCM kwamba wanaCCM wajitokeze kushawishi wenzao wanaodhani wanafaa kuwania urais.
 
Pamoja na utata huo unaozunguka suala la Lowassa, bado Membe amewaambia wenzake kwamba endapo ataamua kugombea, angetamani kinyang’anyiro hicho kimshirikishe Mbunge huyo wa Monduli ili “mzizi wa fitina” kuhusu suala hilo la nani ana nguvu ndani ya CCM uweze kukatwa.

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top