Habari Kali
Loading...

TIBA YA FANGASI WANAOSHAMBULIA SEHEMU ZA SIRI

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >


Wiki iliyopita tulieleza kwa urefu kuhusu tatizo la fangasi kwa wajawazito baada ya kueleza tatizo la kuwashwa sehemu za siri kunakotokana na fangasi  na tukaahidi kwamba tiba na ushauri tutafafanua leo.
Kabla ya kueleza tiba tufafanue kwamba kuna baadhi ya mambo yanayosababisha watu kuwashwa sehemu hizo nyeti kama vile kuwa na fangasi tuliowataja  katika matoleo yetu yaliyopita.
Wengine huwashwa kutokana na kutumia dawa za antibayotiki kwa muda mrefu. Dawa za antibayotiki ni kama, ampicillini, amoxyclini, ciproflaxine, doxylline, erythromycine, gentamcycine na nyingine nyingi hivyo basi, jamii isitumie ovyo dawa hizi bila ushauri wa daktari.
Kutumia dawa hizo husababisha fangasi kwani huua wadudu wote wanaolinda mwili na kuacha sehemu za siri kukiwa hakuna kinga. Sababu nyingine ni unene kupita kiasi. Mtu akinenepa anaweza kupata fangasi kwa sababu unene husababisha jasho sehemu za siri na kuongeza unyevunyevu sehemu hizo, pia michubuko kutokana na kubanwa na chupi.
Sababu nyingine ni utumiaji wa dawa ya jamii ya steroid, dawa hizi ni kama prednisoline, hydrocortisone, dexameltasone na nyingine nyingi. Hizi nazo hupunguza kinga ya mwili na kusababisha fangasi kuzaliana kwa wingi sehemu nyeti.
Pia kuna magonjwa yanayosababisha kupungua kwa kinga nayo ni kisukari, Ukimwi na magonjwa mengine yanayopunguza kinga ya mwili na kusababisha fangasi.
Kuwepo na joto kupita kiasi na kuvaa nguo za ndani ambazo hazijakauka pia husababisha fangasi sehemu za siri.
Dalili
Dalili kwa maradhi ya fangasi hutofautiana kati ya mtu na mtu ila dalili kubwa ni kutokwa na majimaji meupe wakati mwingine kama mgando wenye rangi ya njano ukiwa umeambatana na muwasho  sehemu za ndani au kwenye mashavu ya sehemu za nje za siri za mwanamke.
Nje ya sehemu hizi za siri hutokea wekundu na maumivu wakati wa kukojoa au wakati wa tendo la ndoa pia mgonjwa atajikuta akikojoa mara kwa mara.
VIPIMO
Wote wenye dalili hizo wanashauriwa kwenda kwa daktari ambapo baada ya kumuona ataanza kumchunguza mgonjwa sehemu yake ya siri ambao kitaalamu huitwa PV exam.
Daktari pia atachunguza kama kuna uchafu wowote unaotoka, wingi wake, rangi yake, harufu yake, na mgonjwa awe huru kumsimulia daktari tatizo lake kama anaona haya niliyoyataja.
Mgonjwa atachunguzwa kama ana mitoki sehemu za siri na daktari ataangalia shingo ya kizazi, sehemu ya haja kubwa kama kuna  bawasiri (haemorrhoids) nk.
Itaendelea wiki ijayo.

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top