BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
Watafiti wakitoa sampuli za damu kutoka kwa sokwe mtu katika utafiti wa Ukimwi huko Gabon. Picha ya Mtandao
Watafiti
katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba cha Temple, Marekani wamegundua
dawa ya kuangamiza Virusi Vya Ukimwi (VVU) ambayo ni ya uhakika zaidi
ukilinganisha na zilizowahi kupatikana katika tafiti za awali duniani.
Dawa yao inaweza kutumika kwa tiba ya wanaoishi na VVU na kinga kwa wale ambao bado hawajaambukizwa.
Mmoja
wa watafiti hao, Dk Kamel Khalili aliwaambia waandishi wa habari juzi
mjini Philadelphia, Marekani kuwa tofauti na utafiti mwingine, wao
wamegundua namna ya kukiondoa kirusi kilichoingia kwenye kinasaba (DNA)
ndani ya CD4 na kukitoa nje na hatimaye kukiua.
Alisema dawa hiyo inafanya kazi hiyo bila kuathiri seli za mwili wa binadamu.
Dk
Khalili alisema ugunduzi wao ni wa hali ya juu zaidi kwa sababu
teknolojia ya kutengeneza dawa hiyo ni tofauti na nyingine zilizokwisha
kugunduliwa ambazo hazina uwezo wa kupenya ndani ya seli za binadamu,
bali kuathiri tu VVU vilivyopo nje yake, ndani ya mfumo wa damu.
“Dawa
yetu inakivuta kirusi nje ya seli (CD4) bila kuiathiri seli yenyewe na
kukiua. Hivyo dawa hii itatumika kwa muda fulani na kuua virusi vyote
mwilini na hakuna haja ya kuitumia wakati wote kama ilivyo dawa ya
kufubaza VVU (ARV).”
ARV
huangamiza VVU vilivyopo kwenye damu na kuendelea kuviacha hai vile
ambavyo tayari vimeingia ndani ya CD4, hivyo kufanya virusi kuzuka upya
pindi mwathirika anapoacha kutumia dawa.
Mmoja
wa wataalamu katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu
Kituo cha Mbeya (NIMR-MMRC), Clifford Majani ameuelezea utafiti huo
kama mwanga mpya katika teknolojia ya kukabili VVU.
“Kama
imepatikana teknolojia ya kukiondoa kirusi ndani ya seli ni hatua nzuri
ya kukabili VVU. Hili lilionekana kuwa gumu mwanzoni,” alisema Majani.
Alisema
imekuwa vigumu kuua kirusi kikiwa ndani ya seli na hata baadhi ya
wanasayansi wamejaribu kutengeneza dawa itakayotambua seli
zilizoathirika ili ziuawe lakini hilo likawa gumu.
“Inaweza
ikapatikana dawa ya namna hiyo (inayoua seli zilizoathirika) lakini
ikawa inaathiri vitu vingine ndani ya mwili. Hilo halikubaliki. Kikubwa
katika ugunduzi huo ni dawa kuweza kukifuata kirusi kinakojificha na
kukiondoa, jambo ambalo dawa nyingi zimeshindwa zikiwamo ARV,” alisema.
Hata hivyo, Majani alisema changamoto ambayo inaweza kujitokeza katika majaribio ya dawa hiyo ni usalama wakati wa matumizi.
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out:
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Filed Under:
Kimataifa
Friday, 22 August 2014