WAKATI
Saluti5 ilipofanya ziara ya kwenda Masaki kijijini kwa mwimbaji Muhidin
Maalim Gurumo aliyefriki Jumapili, ilipata mambo mengi mahsusi kutoka
mwa gwiji huyo.
Marehemu
Gurumo kwa maisha yake yote alikuwa na ulemavu wa jicho moja lakini
hakuna mwanamuziki wala mdau au mwanahabari aliyekuwa anajua sababu ya
madhila hayo ya mzee wetu mpendwa.
Gurumo akaileza Saluti5 mbele ya mdau mkubwa wa muziki Juma Mbizo sababu ya jicho lake kupotea.
Ilikuwa
jambo la kusisimua sana. Alitupeleka hadi mbele ya nyumba yake na
kukutana na mti wa mwembe na kisha akasema: “Leo nataka niwaambie jambo
moja ambalo sijui kama yupo mtu anayelijua.
“Huu mti una historia kubwa kwangu. Hapa ndipo nilipopoteza jicho langu nikiwa na umri wa miezi mitatu.
“Mama
yangu alinilaza kwenye kivuli cha mti huu kisha akaenda kuendelea na
shughuli zake. Bahati mbaya likaanguka tawi na kutua kwenye jicho langu.
“Nilisimuliwa
kuwa juhudi za hospitali hazikusaidia kitu, nikapoteza jicho langu,”
alimaliza Gurumo na kisha akataka arekodiwe kwa njia ya video ili
tujipatie kumbukumbu adimu.
Baadae tutakuwekea video ya Gurumo akisimulia namna alivyopoteza jicho lake.
CHANZO: Saluti5.com
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >