Rais Jakaya Kikwete amesema ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa
adabu unaoonyeshwa na baadhi ya Watanzania kuwatukana, kuwadhihaki na
kuwakejeli waanzilishi wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na
Sheikh Abeid Amani Karume.
Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi alipokuwa
kwenye mahojiano maalumu na wahariri wa baadhi ya vyombo vya habari (wa
Mwananchi hawakuwapo) ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano.
Kauli hiyo ilikuwa ni jibu la moja ya maswali
alilokuwa ameulizwa na wahariri hao kuhusu matusi, kejeli na dhihaka
ambazo zimekuwa zinaonyeshwa na wajumbe wachache wa Bunge Maalumu la
Katiba juu ya waasisi hao wa Tanzania na wabunifu wakuu wa Muungano wa
Tanzania.
“Ni kukosa adabu na ni utovu mkubwa wa nidhamu kwa
Mtanzania yeyote kuwatukana, kuwadhihaki au kuwakejeli waasisi wa Taifa
letu. Hawa ni watu ambao waliifanyia nchi yetu mambo makubwa,” alisema
Rais Kikwete na kuongeza:
“Mzee Karume yule aliongoza Mapinduzi yaliyoondoa
dhuluma na uonevu pale Visiwani. Waafrika walio wengi walikuwa wanaonewa
sana pale Tanzania Visiwani, pengine watu wamesahau, lakini hata pale
walipokuwa wanashinda uchaguzi, bado walikuwa hawapewi nafasi ya
kuongoza maisha yao wenyewe.”
Rais alisisitiza kuwa ni ukosefu wa adabu kwa
yeyote kumshutumu mtu aliyejitolea kiasi hicho ili kubadilisha mfumo
dhalimu na kujenga maisha na mazingira ya maisha bora kwa wengi.
“Mzee Nyerere yule ametuachia Taifa moja,
lililoungana, lenye umoja, lenye amani na mshikamano. Misingi ambayo
aliijenga yeye ndiyo imeendelea kuongoza Taifa letu kwa miaka yote hii,”
alisema.
Wakati huo huo, Rais Kikwete alipokea rasmi tuzo
ya Kiongozi Bora wa Maendeleo Afrika –kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje
na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe aliyeipokea kwa niaba yake
huko Marekani, Aprili 9, mwaka huu.
Rais Kikwete alisema amepokea tuzo hiyo na
amewazawadia Watanzania wote, kwa sababu wao ndiyo waliochangia
maendeleo yaliyomwezesha kupata heshima hiyo.
“Napokea Tuzo hii kwa niaba ya Watanzania wote.
Aidha, naitoa kwa Watanzania kwa sababu, hata kama nimekuwa kiongozi,
ukweli ni kwamba mafanikio na maendeleo yote yaliyopatikana hadi
kutunukiwa tuzo hii, yametokana na juhudi zetu za pamoja,” alisema.
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >