Habari Kali
Loading...

Mzimu wa Zitto Kabwe wamfiksha katibu wa CHADEMA , CCM

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

MZIMU wa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe umeelezwa kumkimbiza hadi Chama Cha Mapinduzi (CCM) Katibu wa Chadema jimbo la Mufindi Kusini, Emannuel Ngwalanje.
 
Hatua ya Ngwalanje kujitoa Chadema na kujiunga na CCM imeelezwa na baadhi ya wafuasi wa Chadema kuwa ni pigo kubwa kwa chama hicho.
 
Akizungumzia kujitoa kwa Ngwalanje, mwanachama wa Chadema Michael Ngimbusi alisema; “Ngwalanje alikuwa nguzo kuu ya Chadema wilayani Mufindi, aliogopwa na wana CCM, hiyo ikiwa ni kutokana na uwezo wake mkubwa wa kushawishi na kujenga hoja.
 
Katika kipindi cha zaidi ya miaka minne ambacho Ngwalanje amekuwa Katibu wa Chadema jimbo la Mufindi Kusini ameweza kushawishi zaidi ya wakazi 600 katika maeneo mbalimbali jimboni humo kujiunga na chama hicho.
 
Katika mkutano wa mapokezi yake uliofanyika kijijini kwake Kimilinzowo kata ya Itandula alisema; “Kazi ya kuibomoa Chadema haitaishia katika wilaya ya Mufindi pekee, bali nitaiendeleza hadi Jimbo la Iringa Mjini linaloongozwa na Mchungaji Peter Msigwa kupitia Chadema.” Ngwalanje alisema utawala mbovu na matumizi mabaya ya fedha za ruzuku utaisambaratisha Chadema katika kipindi kifupi kijacho.
 
Alisema chama hicho kinapata fedha nyingi zinazotokana na ruzuku ya serikali na michango ya wanachama, wafuasi na marafiki zake wa ndani na nje ya nchi lakini zimekuwa zikiwanufaisha wachache.
 
Alisema wakati kundi kubwa la viongozi wa chama hicho likifanya kazi kwa kujitolea, kundi la wachache walioko makao makuu wamekuwa wakitafuna fedha hizo bila woga huku wakiwatishia wanaohoji.
 
Alisema demokrasia inayohubiriwa kutafutwa na chama hicho nchini ina walakini kwa kuzingatia kwamba ndani ya chama hicho zipo nafasi za uongozi ambazo kwa wengine ni uhaini kuziwania.

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top