Habari Kali
Loading...

TAIFA STARS YAREJESHA ENZI ZA RAHA, YAIFUMUA BENIN 4-1 TAIFA

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
TANZANIA imepata ushindi mnono dhidi ya Benin, wa mabao 4-1 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Hakizimana Louis, aliyesaidiwa na Simba Honore na Niyitegeta Jean Bosco wote wa Rwanda, hadi mapumziko, Stars tayari ilikuwa inaongoza mabao 2-0.
Mabao hayo yalifungwa na beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ dakika ya 16 na kiungo Amri Kiemba dakika ya 39.
Cannavaro alifunga bao hilo kwa kichwa baada ya kuruka katikati ya msitu wa mabeki wa Benin kuunganisha kona ya Erasto Edward Nyoni kutoka kulia.
Juma Luizio (katikati) akipongezwa baada ya kufunga bao la nne

Kiemba alifunga bao zuri mno akipokea pasi ya Mwinyi Kazimoto na kuanza ‘kuwapunguza’ mabeki wa Benin kabla ya kumchambua kipa wa Benin Farnoue Fabien.
Nyota wa West Bromwich Albion, Sessegnon Stephanne alikuwa mwiba kwa safu ya ulinzi ya Stars, lakini hata hivyo walifanikiwa kumdhibiti asisababishe madhara.
Kipindi cha pili, Benin walianza na mabadiliko wakimpumzisha kipa wao wa kwanza mwenye umbo kubwa, Farnoue Fabien na kumuingiza Allagbe Saturnin.
Hata hivyo, kipa huyo alitunguliwa sawa na mwenzake, mabao mawili ndani ya dakika 45, huku Benin ikifanikiwa kupata bao la kufutia machozi.
Nadir Haroub 'Cannavaro' baada ya kufunga bao la kwanza
Amri Kiemba kushoto baada ya kufunga bao la pili
Kikosi cha Stars kilichoanza leo
Thomas Ulimwengu akimtoka beki wa Benin

Mshambuliaji wa TP Mazembe, Thomas Ulimwengu aliifungia Stars bao la tatu dakika ya 49 akimalizia krosi fupi ya Mrisho Ngassa aliyemtoka vizuri beki wa Benin.
Mshambuliaji wa ZESCO United ya Zambia, Juma Luizio aliyetokea benchi kuchukua nafasi ya Ngassa, aliifungia Stars bao la nne akimalizia kazi nzuri ya Ulimwengu aliyemtoka beki wa Benin.
Benin ilipata bao la kufutia machozi kupitia kwa Suanon Fadel dakika ya 90.
Stars, leo ikitumia mfumo wa 3-4-3 ilicheza vizuri na kutawala mchezo kwa kiasi kikubwa na ingeweza kupata ushindi mnono zaidi- kama ingetumia vyema nafasi nyingine ilizotengeza.
Kikosi cha Tanzania kilikuwa; Mwadini Ali, Shomary Kapombe, Nadir Haroub ‘Cannavaro’/Said Mourad dk75, Erasto Nyoni, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba/Salum Abubakar ‘Sure Boy’dk58, Haroun Chanongo/Said Ndemla dk77, Mrisho Ngassa/Juma Luizio dk60 na Thomas Ulimwengu/Khamis Mcha ‘Vialli’ dk86.
Benin; Farnoue Fabien/ Allagbe Saturnin dk46, Tossavi Eric, Ore Fortune/Dalmeida Sessy, Badarou Nana, Ogouchi Jean, Adeoti Jordan, Mama Seibom, Sessegnon Stephanne, Pote Mickael, Djigla David/Suanon Fadel dk49 na Dossou Jodel/Adudou Mohammed dk53.  

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top