Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma, Jafari Mohamed amewasihi wanawake walioolewa kuwajibika katika masuala ya unyumba kama maandiko ya dini yanavyoelekeza.
Kamanda huyo alitoa wito huo
baada ya kutakiwa kutoa taarifa ya kukatwakatwa na panga kwa mwanamke
mmoja kutokana na kukataa kufanya tendo la ndoa na mumewe kwa sababu ya
uchovu.
Kamanda Mohamed alisema alikuwa hajapata
taarifa za kutokea tukio hilo, lakini akashauri wanawake walioolewa
kuwajibika katika masuala ya unyumba ili kupunguza migogoro ya ndoa.
Mwanamke
huyo mkazi wa Sigunga wilayani Uvinza, Jasmin Kassim alilazimika
kufanyiwa upasuaji kwenye Hospitali ya Misheni ya Heri wilayani Kasulu
kuunga mifupa ya mikono yake baada ya kushambuliwa na mumewe.
Akisimulia
mkasa huo juzi, Kassim alidai kuwa Oktoba 29 saa 4:00 usiku, baada ya
kumaliza kula chakula alikwenda chumbani kulala ndipo mumewe alipotaka
haki yake ya ndoa, lakini alimwambia kwamba alikuwa amechoka.
“Kilichonikuta
baada ya kumkatalia alitoka nje na alirudi akiwa ameshika panga, ghafla
akaanza kunipiga kisha kunikatakata katika mikono yote miwili.
“Nilipozinduka nikajikuta nipo zahanati ya kijiji, nikashonwa zaidi ya nyuzi tano,” alidai Kassim.
Kassim
alisema kutokana na majeraha hayo alihamishiwa Hospitali ya Rufaa ya
Maweni iliyopo Ujiji ambako alilazwa.
Baada ya uchunguzi iligundulika kuwa mifupa ya mikono imeachana na ndipo akafanyiwa upasuaji kwa mara ya pili.
Baada ya uchunguzi iligundulika kuwa mifupa ya mikono imeachana na ndipo akafanyiwa upasuaji kwa mara ya pili.
BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >