Habari Kali
Loading...

Wazazi wa yule mtoto aliyefungiwa ndani ya Box wasota rumande

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >
BABA mzazi pamoja na walezi wa mtoto anayedaiwa kufichwa kwenye boksi kwa takribani miaka mitatu, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mjini Morogoro na kusomewa mashitaka ya kula njama na kufanya ukatili dhidi ya mtoto huyo.
Rashid Mvungi (47), mkazi wa Lukobe na mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro, ambaye ni baba wa mtoto huyo pamoja na wanandoa Mariamu Said (38) na mumewe, Mtonga Omar (30) walifikishwa mahakamani jana.

Mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Mary Moyo, Wakili wa Serikali, Sunday Hyera kwa kushirikiana na Mwendesha Mashitaka wa polisi, Anganile Msiani walidai washitakiwa walitenda makosa hayo kati ya Desemba mwaka 2010 na Mei mwaka huu katika eneo la Kiwanja cha Ndege, mjini Morogoro.
Walidai katika kipindi hicho, washitakiwa wakiwa walezi wa mtoto huyo, walimfanyia ukatili wa kumtelekeza na kumpa malezi akiwa ndani ya boksi na hivyo kumsababishia magonjwa. Walitaja maradhi yaliyomkumba mtoto huyo akiwa ndani ya boksi pamoja na utapiamlo, maumivu ya kifua na mvunjiko wa mifupa katika maeneo ya mikono na miguu.
Mawakili hao walidai upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuiomba mahakama kutaja tarehe ya kuanza kusikilizwa.
Wakili wa Serikali, Hyera alidai mahakamani kwamba upande wa Jamhuri hauna kipingamizi kuhusu dhamana kwa washtakiwa.
Hakimu Moyo alisema dhamana kwa washitakiwa iko wazi ,lakini kwa masharti ya kila mmoja kuwa na wadhamini wawili watakaosaini bondi ya Sh milioni tano kila mmoja.
mtoto aliyefungiwa
Alisema sharti lingine ni kwa wadhamini kuwa na barua kutoka kwa waajiri wa kuaminika au serikali za mitaa.
Washtakiwa walishindwa kutimiza masharti hayo, hatua iliyowafanya warejeshwe rumande. Kesi hiyo imeahirishwa hadi Juni 9 mwaka huu kwa ajili ya usikilizaji wa awali.

BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

Ugandan socialite Zari is undeniably hot and Diamond Platnumz cannot be blamed for going kookoo for her, Besides her looks, she is also ambitious and rich. Born on 23rd of September 1980, Zari grew up in Jinja and after high school she moved Kampala where she performed karaoke in hang-outs. She later moved to London and acquired a diploma in cosmetology. She now lives in South Africa where she runs cosmetics shop while pursuing a career in music. She shared some of her never before seen photos from back in the day and she was still hot. Check her out: BONYEZA HAPA CHINI KUANGALIA MOVIE MPYA ZA BONGO== >

TOA MAONI YAKO KUHUSU HABARI HII.. HAPA CHINI
Newer Posts Older Posts
© Copyright DONDOO ZA HABARI | Designed By Code Nirvana
Back To Top